MO: Kailima awatoa hofu Watanzania

Naibu katibu mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani awatoa hofu Watanzania kuwa nchi ipo salamaL licha ya kutokea kwa tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara Mohammed Dewji.

Naibu katibu mkuu huyo amesema hayo mkoani Simiyu ambapo amesema tukio hilo haliwezi kuharibu sifa ya nchi nzima kwani matukio kama haya hutokea pia nchi nyingine duniani kote.

Katika hatua nyingine, Naibu katibu mkuu huyo amekabidhi nyumba 10 kwa Jeshi la Polisi mkoani Simiyu wilayani Maswa.

Nyumba hizo zilikuwa zikikaliwa na wakandarasi wa Barabara ya Maswa – Mwigumbi ambao wamekamilisha kazi zao.

Zaidi ya askari 33 wanatarajiwa kuishi ndani ya nyumba hizo, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais John Magufuli aliyoitoa wakati akiwa waziri wa Ujenzi.

Unaweza kuangalia pia

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha mazingira ya ufanyaji biashara za huduma za kifedha ili kuvutia uwekezaji wa ndani na nje kwa kuwa maendeleo endelevu ya taifa hayawezi kufikiwa bila ushiriki thabiti wa sekta binafsi

Amesema kuwa sekta ya fedha ni kichocheo kikubwa katika ukuaji wa Uchumi na ustawi wa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *