MO: Kailima awatoa hofu Watanzania

Naibu katibu mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani awatoa hofu Watanzania kuwa nchi ipo salamaL licha ya kutokea kwa tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara Mohammed Dewji.

Naibu katibu mkuu huyo amesema hayo mkoani Simiyu ambapo amesema tukio hilo haliwezi kuharibu sifa ya nchi nzima kwani matukio kama haya hutokea pia nchi nyingine duniani kote.

Ad

Katika hatua nyingine, Naibu katibu mkuu huyo amekabidhi nyumba 10 kwa Jeshi la Polisi mkoani Simiyu wilayani Maswa.

Nyumba hizo zilikuwa zikikaliwa na wakandarasi wa Barabara ya Maswa – Mwigumbi ambao wamekamilisha kazi zao.

Zaidi ya askari 33 wanatarajiwa kuishi ndani ya nyumba hizo, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais John Magufuli aliyoitoa wakati akiwa waziri wa Ujenzi.

Ad

Unaweza kuangalia pia

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetenga zaidi ya shilingi bilioni 250 katika mwaka wa fedha 2024/25 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa na vifaa tiba kwa vituo vyote vya kutolea huduma za afya ya msingi katika Halmashauri zote 184 nchini

Taarifa hii imetolewa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI anayeshughulikia …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *