Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dokta Mary Mwanjelwa

MFUMO MPYA WA TAARIFA ZA WATUMISHI WA UMMA KUANZA KUTUMIKA

  • Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dokta Mary Mwanjelwa amesema wizara ipo katika hatua ya mwisho ya kuwa na mfumo mpya wa kupata taarifa za watumishi wa umma kote nchini ikiwa ni pamoja na kituo cha kutoa huduma kwa pamoja.
  • Naibu Waziri Mwanjelwa amesema hayo katika mahojiano katika kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na TBC ambapo amesema kuwa mfumo huo utawezesha kupatikana kwa taarifa za watumishi kwa urahisi.
  • Katika hatua nyingine Dokta Mwanjelwa amewataka waajiri kuwa na utaratibu wa kupeleka taarifa zilizo sahihi kuhusiana na watumishi wao ili kuondoa ucheleweshwaji wa kupanda madaraja kwa watumishi.
  • Amesema mara nyingi wizara imekuwa ikilaumiwa kutokona na ucheleweshwaji wa masuala mbalimbali jambo ambalo huanzia katika ofisi zao na kuwataka waajiri kubadilika.
  • Msikilize Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dokta Mary Mwanjelwa akitoa ufafanuzi
[soundcloud url=”https://api.soundcloud.com/tracks/559856220″ params=”color=#ff5500&auto_play=false&hide_related=false&show_comments=true&show_user=true&show_reposts=false&show_teaser=true&visual=true” width=”100%” height=”300″ iframe=”true” /]

 

 

 

 

Ad

Unaweza kuangalia pia

RAIS MAGUFULI AIPONGEZA MAHAKAMA NA WADAU KWA MAFANIKIO MAKUBWA

Rais  Dkt. John  Magufuli ameipongeza Mahakama na wadau wake kwa hatua kubwa za kimaendeleo zilizopigwa …

Oni moja

  1. Asante sana,na Hongera Sana kwa Serikali ya Awamu ya Tano.Binafsi Nafanya kazi kwa Furaha kubwa,kwa Bidii ,nikistajabu na kufurahishwa na mambo mapya ya kuijenga Tanzania Mpya.Rais wetu,Mteule Toka kwa Mungu na Uongozi wake Mzima.Tunawapongezeni mno,mno kwa kazi nzuri mno zinazoendelea kwa Manufaa ya Wa Tanzania Nikiwa Kama Mtumishi nishukuru kwa mfumo mpya,Maana utasaidia Mambo Mengi.Asanteni Sana Mungu awaneemeshe na Awabariki Sana Asante Sana.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *