Madaktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma wakimfanyia mgonjwa uchunguzi wa mishipa ya damu ya moyo (coronary angiogram) kwa kutumia mtambo wa Cathlab. Mtambo huo wa Cathlab ambao ni maabara ya uchunguzi na matibabu ya mishipa ya moyo umeanza kufanya kazi kwa mara ya kwanza leo na kuweza kutoa huduma kwa wagonjwa watano.

MADAKTARI BINGWA WA MAGONJWA YA MOYO WA JKCI NA BENJAMINI (BMH) WAANZA UCHUNGUZI WA MISHIPA YA DAMU YA MOYO

Mkurugenzi Mtendaji wa  Taasisi ya Moyo
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma pamoja na timu ya wataalamu wa Taasisi hiyo kwa ajili ya kuanza kutoa huduma ya upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kwa kutumia mtambo wa Cathlab (Catheterization) kupitia tundu dogo linalitobolewa kwenye paja. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa BMH Dkt. Alphonce Chandika.
Mkurugenzi Mtendaji wa  Taasisi
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwafundisha wataalamu wa afya wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma kuhusu madhara ya moyo kushindwa kufanya kazi (Heart Failure) kabla ya kuanza kwa uchunguzi wa mishipa ya damu ya moyo (coronary angiogram) kwa wagonjwa kupitia mtambo wa Cathlab. Mtambo huo wa Cathlab ambao ni maabara ya uchunguzi na matibabu ya mishipa ya moyo umeanza kufanya kazi leo na kuweza kutoa huduma kwa wagonjwa watano.
Madaktari Bingwa
Madaktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma wakiwa na nyuso za furaha mara baada ya kumaliza kufanya uchunguzi wa mishipa ya damu ya moyo (coronary angiogram) kwa mgonjwa wa kwanza kwa kutumia mtambo wa Cathlab. Mtambo huo wa Cathlab ambao ni maabara ya uchunguzi na matibabu ya mishipa ya moyo umeanza kufanya kazi leo na kuweza kutoa huduma kwa wagonjwa watano.
Ad

Unaweza kuangalia pia

WAZIRI UMMY AWATAKA WAZAZI KUWEKEZA KATIKA AFYA ZA WATOTO

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amewataka wazazi kuwekeza …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *