POSTA MNAWAJIBU WA KURAHISISHA UTOAJI WA HUDUMA KIDIGITALI – DKT. YONAZI

 
  • Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imesema kuwa Shirika la Posta Tanzania linawajibu wa kuisaidia Serikali katika kuharakisha maendeleo kwa kurahisisha utoaji wa huduma za barua, nyaraka, vipeto na vifurushi ndani na nje ya nchi kwa kwenda kidigitali ambako dunia ndio iko huko. duma
  • Hayo ameyasema na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano -Mawasiliano Dkt.Jimmy Yonazi wakati alipomwakilisha Waziri wa Wizara hiyo katika siku ya kilele cha maadhimisho ya miaka 145 ya Umoja wa Posta duniani.
  • Dkt. Yonazi amesema kuwa shirika hilo limekuwa likirahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha za uwakala hasa maeneo ambayo hayafikiwi kirahisi na Kampuni pamoja na taasisi zinazotoa huduma za kibiashara.
  • Dkt. Yonazi amesema shirika linajukumu la msingi la kutoa huduma za posta kwa watu wote hivyo ni muhimu likaendelea kuboresha mikakati yao ili liweze kuwafikia watanzania kote nchini ikienda sambamba na huduma bora.
  • “Tupo Serikali ya awamu ya tano inayowataka watu kufanya kazi, shirika hili ambalo linamilikiwa na serikali kwa asilimia 100 lina wajibu wa kufuata kauli mbiu hiyo kwa vitendo, kwa kuhakikisha huduma zinazotolewa ni bora kwa wateja mnaowahudumia ” amesema.
  • Amesema shirika hilo haliwezi kukwepa kuwa moja ya watumiaji wakuu wa mifumo ya kompyuta na mitandao kwani ndiko dunia ilipo kwa sasa na biashara inafanyika katika mitandao .
  • Naye Kaimu Posta Masta Mkuu wa Shirika hilo, Mwanaisha Said amesema wamejizatiti na kuboresha baadhi ya huduma zao ambazo nyingi kwa sasa zinafanyika kidigitali katika kufanikisha maendeleo endelevu.
  • Said amesema kwa mwaka huu wamepata mwitikio mkubwa kutoka Tanzania bara na visiwani katika kushiriki shindano ambapo jumla ya wanafunzi 1881 walijitokeza ikilinganishwa na 850 walioshiriki mwaka jana ikiwa na kutaka wanafunzi washiriki Shindano la Afrika la uandishi wa habari.
  • Washindi katika shindano hili wa kwanza ni Joan Erasto kutoka shule ya Sekondari ya Binza iliyopo Simiyu, wa pili ni Grace Kahimba kutoka Shule ya msingi ya St Ann’s ya Morogoro na mshindi wa tatu ni Hasnein Rizwan wa Shule ya Almuntazir Boys Seminari ya jiji Dar es Salaam.
  • Mwenyekiti wa bodi ya Shirika hilo, Dk. Harun Kondo amesema shirika hilo limesimama na kuzalisha faida kwa sasa kutokana na mshikamano uliyopo kati ya bodi na wafanyakazi. Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Ad

Unaweza kuangalia pia

BANDARI YA DAR ES SALAAM INAPANUKA NA KUIMARIKA: HATUA MUHIMU KWA UCHUMI WA TANZANIA

Bandari ya Dar es Salaam ni kitovu muhimu cha biashara na uchumi wa Tanzania, na …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *