Maktaba ya Kila Siku: February 4, 2020

TUNAWEKA MIKAKATI YA KUPANDA MITI ZAIDI YA MILIONI 1 KATIKA MLIMA KILIMANJARO – WAZIRI ZUNGU

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Azzan Zungu amesema Serikali inatarajia kuweka mikakati ya kupanda miti zaidi ya milioni moja kwenye eneo la Mlima Kilimanjaro ili kulinda barafu iliyopo nchini. Pia amewataka wananchi kuacha tabia ya kukata miti na kuitumia kama fursa ya …

Soma zaidi »

WAKAZI WA PEMBEZONI MWA BAHARI WAELIMISHWA ATHARI ZA MAGENDO

Wakazi na wafanyabiashara waishio pembezoni mwa fukwe za Bahari ya Hindi katika kata za Somangila, Kimbiji na Pemba Mnazi zilizopo Wilaya ya Kigamboni jijini Dar es Salaam wameelimishwa kuhusu athari za magendo yanayopitishwa kinyume na sheria katika maeneo hayo. Elimu hiyo imetolewa wakati wa kampeni maalum ya kuelimisha wananchi kuhusu …

Soma zaidi »

WAZIRI UMMY AKAGUA JNIA TERMINAL 3 UTAYARI WATUMISHI WA AFYA DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameridhishwa na hali ya ukaguzi wa abiria wanaoingia nchini katika uwanja wa ndege wa Kimataifa cha Julius Nyerere(JNIA) jengo la tatu la abiria-TB3 dhidi ya homa kali ya mafua inayoenezwa na virusi vya Corona. Awali akiwa uwanjani hapo aliweza …

Soma zaidi »

NENDENI MKATANGULIZE UZALENDO KWANZA – RAIS MAGUFULI

Rais Dkt. John Pombe Magufuli amewataka viongozi walioapishwa kufanya kazi kwa kufuata sheria na kanuni za uongozi pamoja na kuwa na   hofu ya Mungu bila kusahau kutanguliza Uzalendo katika kuhakikisha Tanzania inafikia malengo iliyojiwekea. Rais Magufuli Ameyasema hayo leo tarehe 3 Februari 2020 katika hafla ya Uapisho wa Viongozi mbalimbali …

Soma zaidi »

DC CHONGOLO ASITISHA VIBALI VYA UCHIMBAJI MCHANGA MABONDENI KATIKA WILAYA YA KINONDONI

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo amesitisha vibali vya uchimbaji mchanga vilivyotolewa na Bodi ya Maji Bonde la Ruvu kutokana na kuleta madhara ya uharibifu wa mito na kusababisha athari kwenye makazi ya watu katika Halmashauri hiyo. Vibali vilivyositishwa katika ni vile vilivyotolewa kufanya shughuli hizo katika Bonde la …

Soma zaidi »