WAZIRI MKUU AMPONGEZA BONDIA SALIM MTANGO ALIYESHINDA MKANDA WA DUNIA WA UBO

8-01
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpongeza mwanamasumbwi, Salim Mtango wa Tanga ambaye Januari 31, 2020 alifanikiwa kumshinda kwa TKO bondia wa Thailand, Suriya Tarakhun na kunyakuwa mkanda wa dunia wa UBO. Bondia huyo alitembelea bunge jijini Dodoma Februari 6, 2020 kwa mwaliko wa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (mwenye koti la bluu kulia). Wa tatu kushoto ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe na kushoto ni Naibu wake, Juliana Shonza. Kulia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Mendeleo Mijini, Angelina Mabula. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
7-01
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt, Harrison Mwakyembe kwenye viwanja vya bunge jijini Dodoma, Februari 6, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
6-01
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mwita Waitara (kushoto) kwenye viwanja vya bunge jijini Dodoma, Februari 5, 2020. Wa pili kulia ni Mbunge wa Nachingwea, Hassan Masala na wa tatu kulia ni Mbunge wa Lindi, Hassan Kaunje. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
5-01
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama akizungumza na Mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge, bungeni jijini Dodoma, Februari 6, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
4-01
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Uwekezaji), Angellah Kairuki (kushoto) akizungumza na Waziri wa Madini, Doto Biteko, bungeni jijini Dodoma, Februari 6, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
3-01
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Uwekezaji), Angellah Kairuki (kushoto) akizungumza na Waziri wa Nchi , Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mussa Azzan Zungu, bungeni jijini Dodoma, Februari 6, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
2-01
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba , bungeni jijini Dodoma, Februari 6, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
1-01
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Mpwapwa, George Lubeleje, bungeni jijini Dodoma, Februari 6, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Ad

Unaweza kuangalia pia

KATIBU MKUU DKT. ABBASI ASISITIZA MAGEUZI YA KIUTENDAJI KWA MENEJIMENTI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Dkt.Hassan Abbasi amewataka viongozi wa menejimenti wa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *