BALOZI SOKOINE AKUTANA NA MWAKILISHI MKAZI WA UNDP

Balozi Joseph Sokoine Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) ukiongozwa na Bi. Christine Musisi – Mwakilishi Mkazi mara baada ya kukamilika kwa kikao cha mashirikiano baina yao. Wengine katika picha ni wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na UNDP
Balozi Joseph Sokoine Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (kulia) akiwa katika kikao pamoja na ujumbe kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) ukiongozwa na Bi. Christine Musisi ambae ni Mwakilishi Mkazi. Kikao hicho kimelenga kuimarisha ushirikiano katika hifadhi ya Mazingira hususan katika maeneo ya Mabadiliko ya Tabianchi, Uchumi wa Bahari, Nishati endelevu, Hifadhi ya Bioanuai na Ikolojia. Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi za Makamu wa Rais Mtumba – Dodoma.
Balozi Joseph Sokoine Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais akiagana na Bi. Christine Musisi Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) mara baada ya kukamilika kwa mkutano baina yao uliojadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika masuala ya mazingira. Mkutano huo umefanyika katika Ofisi za Makamu wa Rais Mtumba – Dodoma.
Ad

Unaweza kuangalia pia

MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA MRADI WA MAJI SAME MWANGA KOROGWE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri kuhusu maendeleo ya ujenzi wa mradi wa maji Maji wa Same – Mwanga – Korogwe wakati alipotembelea chanzo cha mradi huo eneo la la Nyumba yaMungu Wilaya ya Mwanga wakati akiwa ziarani mkoani Kilimanjaro tarehe 21 Machi 2024. Makamu …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *