DC CHONGOLO AMTAKA MKANDARASI ANAYEJENGA SOKO LA TANDALE KUONGEZA KASI YA UJENZI HUO

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo amemtaka Mkandarasi wa Kampuni ya NAMIS CORPORATE L.T.D ambaye anajenga Soko hilo kuongeza kasi ya ujenzi huo ili Wafanyabiashara waweze kurudi kwenye eneo lao.

Chongolo amesema hayo alipofanya ziara katika soko la Tandale na kuwakuta wafanyabiashara katika mazingira yasiyo rafiki hali inayopelekea usumbufu wa shughuli zao na kumuelekeza mkandarasi huyo kuongeza kasi ya ujenzi huo ili kuondokana na adha inayowakabili.

Ad
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Daniel Chongolo akipata maelezo kutoka kwa Meneja mradi wa Kampuni ya ujenzi NAMIS CORPORATE L.T.D Mhandisi James Msumari namna ambavyo Soko hilo litakavyokuwa.

Amesema lengo la Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inaboresha miundo mbinu yote ya masoko ili wafanyabiashara waweze kufanya biashara na kuendesha maisha yao na hivyo kuziwezesha Halmashauri kufikia malengo hayo.

Amefafanua kuwa mradi huo wa Soko la kisasa unajengwa kwa gharama ya Sh. Bilioni 8.7 fedha ambazo zimetolewa na Serikali kuu na kwamba tayari mkandarasi huyo ameshalipwa fedha zote na hivyo kusisitiza kwamba anapaswa kufanya kazi usiku na mchana ilikukamilisha kazi yake kwa wakati.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Daniel Chongolo akikagua ujenzi wa Soko la kisasa la Tandale leo wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa soko hilo wenye lengo la kujionea namna ambavyo ujenzi huo unavyokwenda.

“Serikali ya Rais Dk. John Magufuli imemlipa mkandarasi pesa zote, hivyo hatudai badala yake sisi ndio tunamdai Soko letu atukabidhi kwa wakati sahihi, wafanyabishara na wananchi wanasubria kwa shauku kubwa sana ukizingatia Soko hili nimuhimu kwa wakazi wa Dar es Salaam, kwasababu litahusika zaidi na biashara ya mazao ya nafaka pamoja na bidhaa nyingine” amesema Chongolo.

Awali Meneja kutoka kampuni hiyo iliyopewa kandarasi ya ujenzi wa Soko hilo Mhandisi James Msumari alimueleza Mhe. Chongolo kuwa ujenzi huo utachukua miezi 12 jambo ambalo alionesha kutokuridhishwa na muda huo na kusema kuwa hakuna sababu ya kutumia muda mrefu kwakuwa fedha wanazo hivyo wanapaswa kukamilisha ujenzi kwa makubaliano yaliyoingiwa.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Daniel Chongolo akitoa maelekezo kwa Meneja mradi wa Kampuni ya ujenzi NAMIS CORPORATE L.T.D Mhandisi James Msumari mara baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa soko hilo.

Kwaupande wake Mhandisi Msumari amesema wamepokea maagizo na wako tayari kuyatekeleza ili waweze kuondoa changamoto zinazowakabilio wafanyabiashara wa eneo hilo.

Ad

Unaweza kuangalia pia

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MKUTANO WA WOMENLIFT HEALTH

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akimsikiliza Maelezo kutoka kwa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *