HALMASHAURI YA CHALINZE MKOANI PWANI YATEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA

Halmashauri ya Chalinze mkoani Pwani imetekeleza maagizo ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa kutengeza madawati 355, meza na viti 221, huku Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete akichangia shilingi milioni 3.67.

Akizungumza wakati wa kupokea madawati hayo zoezi lilofanyika Mioni Wilayani Bagamoyo, Mbunge Kikwete amesema kuwa madawati hayo ni kwaajili ya shule 38, ambapo za sekondari 20 na shule za msingi 18.

Ad

Kikwete amesema kuwa lengo ni kuhakikisha hakuna mwananfunzi anayekaa chini “lengo letu ni kuona wanafunzi wote wanakaa kwenye madawati ili waweze kuandika vizuri wanapokuwa darasani na kuacha kukaa chini darasani” Amesema Kikwete

Madawati hayo yamepokelewa mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani Evarist Ndikilo na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Bi Zainab Kawawa.

Ad

Unaweza kuangalia pia

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MKUTANO WA WOMENLIFT HEALTH

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akimsikiliza Maelezo kutoka kwa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *