NAIBU WAZIRI WA VIWANDA AFANYA MAZUNGUMZO NA WADAU WA SEKTA YA NGUO NCHINI

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Exaud Kigahe akifafanua jambo kwa wazalishaji na waagizaji wa nguo na mavazi hususani vitenge na kanga katika kikao kilichofanyika tarehe Februari 2021 katika ukumbi wa Chuo cha Biashara (CBE ) jijini Dodoma

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Exaud Kigahe amekutana na kufanya mazungumzo na wadau wa sekta nguo na mavazi ili kusikiliza changamoto wanazokutana nazo na mapendekezo yao katika kuboresha na kukuza sekta hiyo.

Akizungumza na wadau hao katika kikao kilichofanyika tarehe 9 Februari 2021 katika ukumbi wa Chuo cha Biashara (CBE ) jijini Dodoma Naibu Waziri aliwaagiza kuwasilisha changamoto walizonazo na rasimu za mipango mikakati ya kuboresha na kuendeleza Viwanda na Biashara katika sekta hiyo ili kukuza uchumi wa nchi.

Ad
Wa kwanza kulia ni Katibu Mtendaji wa Chama cha Wazalishaji Nguo na Mavazi Tanzania TEGAMAT akiwasilisha changamoto zinazowakabili wanachama wake kwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud Kigahe(MB) alipokutana na wadau wa Sekta ya Nguo na Mavazi ili kisikiliza changamoto wanazokutana nazo katika uendelezaji wa Viwanda na biashara ya nguo na mavazi nchini tarehe 9 Februari 2021 katika ukumbi wa Chuo cha Biashara (CBE ) jijini Dodoma

Aidha katika kikao hicho kilichojumuisha wadau ambao ni watengenezaji na waagizaji wa nguo na mavazi kutoka nje ya nchi, wadau hao waliwasilisha changamoto na mapendekezo yao kwa Mhe. Naibu Waziri wakiwa na lengo la kuboresha na kukuza sekta hiyo.

Katibu wa Jumuiya ya Wafanyabishara Tanzania (JWT) Bw. Abdala Mwinyi akiwasilisha changamoto zinazowakabili wafanyabiashara wanaoagiza nguo na mavazi hususan vitenge kwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud Kigahe(MB) katika kikao kilichofanyika tarehe 9 Februari 2021 katika ukumbi wa Chuo cha Biashara (CBE ) jijini Dodoma

Aidha, Serikali imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali katika kuendeleza sekta ya nguo na mavazi nchini ikiwemo kukuza soko la ndani la.bidhaa hizo pamoja na kuandaa na kutekeleza Mkakati wa kuendeleza Sekta ya pamba nguo hadi mavazi ( Cotton to Clothing Strategy C2C 2016 – 2020 ) na kuuhuisha ambapo utekelezaji wake utaanza mwaka 2021 – 2032.

Ad

Unaweza kuangalia pia

MAKAMU WA RAIS ATEMBELEA MRADI WA MAJI SAME MWANGA KOROGWE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri kuhusu maendeleo ya ujenzi wa mradi wa maji Maji wa Same – Mwanga – Korogwe wakati alipotembelea chanzo cha mradi huo eneo la la Nyumba yaMungu Wilaya ya Mwanga wakati akiwa ziarani mkoani Kilimanjaro tarehe 21 Machi 2024. Makamu …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *