KAZI INAENDELEA YA KUSIMIKA MABOMBA YA KUTOLEA MAJI KATIKA MRADI WA UMEME WA JNHPP



Kazi ya usimikaji wa bomba (Draft tube) sehemu ya chini kabisa kwenye mashine nambari 9 imeanza Agosti 17, 2021, katika mradi wa kufua umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), bomba hizo zitatumika kutolea maji katika mitambo ya kufua umeme na kuyarudisha mto Rufiji kwa ajili ya matumizi mengine.

Hii ni hatua kubwa iliyofikiwa baada ya kukamilika kwa uundwaji wa bomba hizi zinazofungwa katika kitako cha msingi wa zege, kilichopo eneo la mita 42.7 juu ya usawa wa bahari.

Usimikaji wa bomba hizi ndio utawezesha kuanza kwa ufungaji wa sehemu za juu za mashine (turbine) na kisha jenereta za kufua umeme.

Ad

Unaweza kuangalia pia

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MKUTANO WA WOMENLIFT HEALTH

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akimsikiliza Maelezo kutoka kwa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *