Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) imesaini hati ya Makubaliano na Kampuni ya FREMU ya nchini Uingereza ili lkuwezesha wafanyabiashara wa Tanzania kuuza bidhaa zao katika soko la Uingereza kupitia Mtandao wa Kampuni ya FREMU.

Makubaliano hayo yamesainiwa na Mkurugenzi wa TANTRADE Bi Latifa Khamis na Mkurugenzi wa Kampuni ya FREMU Ndugu David Mukisa.

Kampuni hiyo inauza bidhaa za vyakula katika soko la Uingereza kutoka nchi mbalimbali za Afrika ikiwemo Uganda, Kenya, Nigeria, Ghana na Rwanda. Kufuatia makubaliano yaliyosainiwa leo, bidhaa za wafanyabiashara wa Tanzania zitaweza kuuzwa katika soko la Uingereza. Katika Hafla ya kusaini Makubaliano hayo, Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE ameushukuru Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza kwa kuwa daraja kati ya TANTRADE na Kampuni ya FREMU. Kwa upande wake Mkurugenzi wa FREMU ameeleza kwamba Jukwaa la Kampuni yake litawezesha wafanyabiashara wa Tanzania kuuza bidhaa zao kwa urahisi katika soko la Uingereza. http://fremu.co.uk

Ad
Ad

Unaweza kuangalia pia

“Tusikubali Kuwa Tarumbeta za Watu Wasio Tutakia Mema”

“Tusikubali kuwa tarumbeta za Watu wasio tutakia mema, Maadili Yetu Mazuri Ya Kitanzania Lazima Tuyatunze, …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *