MZEE PETER FRANCIS MREMA APONGEZA UONGOZI WA RAIS SAMIA KWA UTEKELEZAJI BORA WA MIRADI YA KIMKAKATI

Mzee Peter Francis Mrema, mmoja wa wazee maarufu katika mkoa wa Morogoro, ametoa pongezi za dhati kwa uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa utekelezaji bora wa miradi ya kimkakati nchini.

Mzee Mrema alielezea kuridhishwa kwake na jinsi serikali imekuwa ikiwekeza katika miradi inayolenga kuboresha maisha ya Watanzania.

Ad

Alisisitiza kuwa utekelezaji wa miradi hii, kama vile ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme Ifakara, reli ya SGR, na miradi mingine muhimu, ni hatua kubwa kuelekea maendeleo endelevu ya nchi. Aliongeza kuwa miradi hii imeanza kuonyesha matokeo chanya kwa wananchi, hususan katika sekta za nishati, uchukuzi, na afya.

Katika mazungumzo hayo, Mzee Mrema aliwahimiza Watanzania kuwa wazalendo kwa kutunza na kulinda miradi hii ambayo imejengwa kwa gharama kubwa na kwa ajili ya manufaa ya wote. Alieleza kuwa ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha kuwa miradi hiyo inaendelea kutoa huduma bora kwa muda mrefu.

“Serikali inatekeleza miradi hii kwa bidii kubwa, lakini ni jukumu letu kama Watanzania kuitunza na kuilinda. Ni kupitia uzalendo wetu tutahakikisha kuwa miradi hii inakuwa na manufaa kwa vizazi vijavyo,” alisema Mzee Mrema.

Pongezi hizi na wito wa Mzee Mrema zimepokelewa kwa shangwe na wananchi wa Morogoro, ambao wanaendelea kushuhudia mabadiliko makubwa kutokana na miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali. Wananchi wanatarajia kuwa na ushirikiano zaidi kati ya serikali na jamii katika kuhakikisha kuwa miradi hii inaleta tija inayotarajiwa kwa taifa.

Ad

Unaweza kuangalia pia

“Tusikubali Kuwa Tarumbeta za Watu Wasio Tutakia Mema”

“Tusikubali kuwa tarumbeta za Watu wasio tutakia mema, Maadili Yetu Mazuri Ya Kitanzania Lazima Tuyatunze, …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *