Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amepokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Jamhuri ya Mali, Mheshimiwa Madou Diallo.

Balozi Diallo amemshukuru Rais Samia kwa mapokezi mazuri na kueleza dhamira yake ya kuendeleza na kukuza mahusiano mazuri kati ya Tanzania na Mali. Amesisitiza kwamba atafanya kazi kwa bidii kuhakikisha kuwa nchi hizi mbili zinanufaika na ushirikiano wao katika nyanja mbalimbali.

Mheshimiwa Diallo, ambaye atakuwa na makazi yake jijini Addis Ababa, Ethiopia, atawakilisha nchi yake ya Mali nchini Tanzania. Tukio hili ni ishara muhimu ya kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Mali.

Ad

Rais Samia amempongeza Balozi Diallo kwa uteuzi wake na kuahidi ushirikiano wa karibu kati ya Tanzania na Mali katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo na kidiplomasia. Vilevile, amemhakikishia Balozi huyo kwamba Tanzania itaendelea kushirikiana na Mali katika kukuza uhusiano wa kirafiki na kuimarisha mshikamano wa kiuchumi na kijamii kati ya nchi hizo mbili.

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na wanadiplomasia, ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa juhudi za Tanzania katika kuimarisha ushirikiano na nchi za kigeni kwa lengo la kukuza maendeleo ya kitaifa na kimataifa.

#MSLAC #SisiNdioWajenziWaTanzaniaYetu #SSH #CCM #KaziIendelee #Nchiyangukwanza #SisiniTanzania #matokeochanya #MSLAC #SamiaSuluhuHassan #ChamaChaMapinduzi #PhilipMpango #wizarayaafya #wizarayaujenzi

Ad

Unaweza kuangalia pia

“Tukamate wajibu wetu tuliopewa na Mungu, wa Kukuza watoto wetu katika maadili mema”.‪@samiasuluhu99‬

Twende tukatunze Watoto wetu vile sisi tulivyotunzwa na Wazazi Wetu katika maadili mema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *