Maktaba ya Mwezi: August 2024

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania katika ziara maalumu ya kuboresha mahusiano nchini Cuba

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Tanzania iko tayari kushirikiana na Serikali ya Cuba kujenga kiwanda kikubwa cha kuzalisha chanjo mbalimbali ikiwemo chanjo ya homa ya ini. Amesema viwanda vya dawa nchini Cuba vikiwemo vinavyotengeneza dawa zinazotokana na mimea tiba vimeiwezesha nchi hiyo kupunguza utegemezi wa kuagiza dawa kutoka …

Soma zaidi »

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Robert Gabriel Mugabe kwa ajilli ya kushiriki Mkutano wa 44 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Harare nchini Zimbabwe

#MSLAC #SisiNdioWajenziWaTanzaniaYetu #SSH #CCM #KaziIendelee #Nchiyangukwanza #SisiniTanzania #matokeochanya #MSLAC #SamiaSuluhuHassan #ChamaChaMapinduzi #PhilipMpango #wizarayaafya #wizarayaujenzi

Soma zaidi »

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwaapisha Mawaziri kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam

Mawaziri hao walioapa ni: Mhe. Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi (Mb.) kuwa Waziri wa Katiba na Sheria; Mhe. William Vangimembe Lukuvi (Mb.) kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu); Mhe. Jenista Joackim Mhagama (Mb.) kuwa Waziri wa Afya; na Mhe. Balozi Dkt. Pindi Hazara …

Soma zaidi »

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameondoka Zanzibar na kuelekea Dodoma leo

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Makamu wa Pili wa Rais, Mhe. Hemed Suleiman Abdallah, ameongoza Watendaji Wakuu wa Serikali kumuaga Rais Dk. Mwinyi. Akiwa Mjini Dodoma, Rais Mwinyi anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika Mkutano wa Baraza Kuu la Kanisa la Tanzania Assemblies of God, Chuo …

Soma zaidi »

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe wa Sekretariet ya Jukwaa la Uchumi Duniani (WEF) wakiongozwa na Mkurugenzi wa Masuala ya Ushirikiano katika Usimamizi na Menejimenti ya Taka za Plastiki Bi. Clemence Schmid, Chamwino Dodoma

Katika mazungumzo hayo, Makamu wa Rais amesema serikali imedhamiria kushirikiana na wadau, sekta binafsi pamoja na jumuiya ya kimataifa katika kupambana na tatizo la taka za plastiki nchini. Amesema uzoefu unaonesha kwamba ushirikiano ni njia bora zaidi itakayowezesha kukabiliana na tatizo hilo kwani yapo maeneo ambayo taka za plastiki hutupwa …

Soma zaidi »

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini, Mhe. Ronald Lamola na Waziri wa Mambo ya Nje wa Madagascar, Mhe. Dkt. Rasata Rafaravavitafika pembezoni mwa Mkutano wa Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Harare, Zimbabwe.

Akizungumza na Mhe. Lamola, Waziri Kombo ameeleza kuwa Tanzania itaendelea kudumisha ushirikiano wa kihistoria na kindugu uliopo baina ya Tanzania na Afrika kusini ili kukuza sekta za kiuchumi ikiwemo biashara, utalii, uwekezaji, elimu, afya na maeneo mengine ya kimkakati kwa maslahi ya pande zote mbili.   Naye Mhe. Lamola ameeleza …

Soma zaidi »

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amepokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Jamhuri ya Mali, Mheshimiwa Madou Diallo.

Balozi Diallo amemshukuru Rais Samia kwa mapokezi mazuri na kueleza dhamira yake ya kuendeleza na kukuza mahusiano mazuri kati ya Tanzania na Mali. Amesisitiza kwamba atafanya kazi kwa bidii kuhakikisha kuwa nchi hizi mbili zinanufaika na ushirikiano wao katika nyanja mbalimbali. Mheshimiwa Diallo, ambaye atakuwa na makazi yake jijini Addis …

Soma zaidi »

RAIS DK. MWINYI; ZANZIBAR KUPUNGUZIWA GHARAMA ZA UENDESHAJI WA MIRADI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameonesha utayari wa Serikali ya Zanzibar kushirikiana na Taasisi ya Mabenki Yasiyo na Mipaka (Bankers without Boundaries) katika kuwekeza kwenye miradi ya kipaumbele ambayo italeta tija kwa nchi. Dk. Mwinyi alitoa kauli hiyo leo, tarehe 14 …

Soma zaidi »