OFISI YA WAZIRI MKUU SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI KIWANDA CHA SAMANI RUANGWA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa rai kwa wawekezaji wachangamkie fursa zilizopo nchini kwa kuangalia maeneo mazuri ya kufanya uwekezaji mpya au kupanua uwekezaji wao. Ametoa rai hiyo (Jumapili, Agosti 16, 2020) wakati akizungumza na wakazi wa Namichiga, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi, waliohudhuria uwekaji wa jiwe la msingi kwenye kiwanda cha …

Soma zaidi »

UONGOZI WA WILAYA YA KIBITI UMETEKELEZA MAAGIZO YA RAIS YA KUJENGA CHOO KATIKA STENDI NDANI YA SIKU SABA

Uongozi wa Wilaya ya Kibiti umetekeleza maagizo ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kujenga choo katika stendi ndani ya siku saba.Hayo yamebainika (Alhamisi, Agosti 13, 2020), mara baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kukagua ujenzi wa choo hicho, Rais Magufuli alitoa agizo la kukamilika ujenzi wa choo hicho tarehe …

Soma zaidi »

WAZIRI MKUU: TAKUKURU HAKIKISHENI WATANZANIA HAWARUBUNIWI

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ihakikishe Watanzania hawarubuniwi ili watumie vizuri utashi wao wa kisiasa kuchagua viongozi bora. “Sote tunatambua kuwa Oktoba, mwaka huu Taifa letu litaendesha Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani… mna jukumu zito la kuhakikisha Watanzania hawarubuniwi na …

Soma zaidi »

SERIKALI IMEENDELEA KUWEKA MIKAKATI ENDELEVU YA KUWAWEZESHA VIJANA KUSHIRIKI KATIKA UJENZI WA UCHUMI WA TAIFA – NAIBU WAZIRI MAVUNDE

Serikali imeendelea kuweka mikakati endelevu ya kuwawezesha vijana nchini kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali ili kuendelea uchumi wa Taifa. Hayo yameelezwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu maadhimisho ya Siku ya Vijana …

Soma zaidi »

TUHAKIKISHE UCHAGUZI WA MWAKA HUU UNAKUWA WA AMANI NA UTULIVU -WAZIRI MKUU MAJALIWA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kila Mtanzania anapaswa kuhakikisha uchaguzi wa mwaka huu unakuwa wa amani na utulivu. Amesema kuwa kiongozi wa nchi, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amewahakikishia watanzania kuwa uchaguzi utakuwa wa huru na haki. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Julai 31, 2020) wakati akishiriki swala na …

Soma zaidi »

WAZIRI MKUU MAJALIWA: ULINZI WA NCHI NI KWA WATANZANIA WOTE

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema suala la ulinzi wa nchi ni la Watanzania wote na siyo la kuwaachia vyombo kama Jeshi la Wananchi, Uhamiaji, Polisi au Magereza. Ametoa kauli hiyo (Jumapili, Julai 19, 2020) wakati akizungumza na wakazi wa Matogoro, wilayani Tandahimba, mkoani Mtwara. “Suala la ulinzi ni letu sote …

Soma zaidi »

SERIKALI YATOA SH. BILIONI 20 KULIPA MADENI YA KOROSHO

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imetoa sh. bilioni 20 za kulipa madeni ya wakulima, wasafirishaji, wapuliziaji dawa na waendesha maghala ya korosho. “Rais Magufuli ametoa fedha hizi kwa ajili ya Tandahimba, Masasi, Mtwara na Kibiti kwa ajili ya waliokuwa wamelipwa nusu, waliolipwa kiasi na wasiolipwa kabisa. Fedha hizi zitaanza …

Soma zaidi »

WAZIRI MKUU: VIJANA, AKINAMAMA, NENDENI MKALIME

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka vijana wa wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi waache kukaa vijiweni na badala yake waanzishe bustani ili kujiongezea kipato. “Biashara ya bustani inalipa sana, yeyote anayetaka fedha, ataipata shambani. Nataka niwasisitize sana twende tukalime, twende shambani. Shamba siyo lazima ulime mahindi, mpunga pekee ama muhogo. Bustani …

Soma zaidi »

WANAWAKE WATAKIWA KUTOKUBALI KUTUMIWA NA WANASIASA KUVURUGA AMANI

Na Mwandishi Wetu, Dodoma. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera, Bunge,Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama amewaasa wanawake kutokubali kutumiwa na vyama vya siasa kama mawakala Waziri Mhagama ametoa wito huo jijini Dodoma wakati akizungumza na umoja wa wanawake viongozi wa vyama vya siasa nchini …

Soma zaidi »

WAZIRI MHAGAMA AZINDUA MPANGO WA UENDELEZAJI WA VIWANDA VIDOGO NA VYA KATI JIJINI DODOMA

NA. MWANDISHI WETU Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amezindua Mpango wa Uendelezaji wa Viwanda Vidogo na vya Kati wenye lengo la kutatua changamoto ya upatikanaji wa ujuzi, masoko na mitaji katika miradi midogo …

Soma zaidi »