Maktaba Kiungo: NAIBU WAZIRI WA MADINI

SERIKALI MKOANI SHINYANGA YAKUSANYA  BILIOINI 1.5 KAMA KODI YA MRABAHA NA ADA YA UKAGUZI KUTOKA KWA WACHIMBAJI

Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Joseph kumburu amesema kuwa utaratibu mzuri uliowekwa kwenye usimamizi wa uzalishaji na biashara ya madini kwa wachimbaji wasio rasmi mkoani Shinyanga umepelekea Serikali kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 1.56 kama kodi ya mrabaha na ada ya ukaguzi kuanzia mwezi Mei, 2019 hadi …

Soma zaidi »

UCHUMI WA TANZANIA WAZIDI KUKUA NA KUIMARIKA

Hali ya uchumi wa Tanzania yazidi kuimarika na kukua  kwa asilimia 6.9 ikiwa ni  takwimu za hadi mwezi Septemba 2019, huku lengo likiwa ni kufikia asilimia 7.0% na 7.1% . Taarifa iliyotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) Januari 20 mwaka huu, inaonesha  kuwa uchumi wa dunia utakua kidogo kutoka …

Soma zaidi »

SERIKALI YAJIZATITI KUIMARISHA USIMAMIZI NA UDHIBITI WA RASILIMALI MADINI

Serikali imedhamiria kuwa na mikakati endelevu ya kusimamia na kudhibiti rasilimali madini ili ilete tija iliyokusudiwa kwa Taifa. Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (Mb) leo Januari 25, 2020 Jijini Dodoma alipokuwa akifungua kikao …

Soma zaidi »

BUNGE KUHARAKISHA UANZISHWAJI SHERIA BODI YA WANAJIOSAYANSI NCHINI

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limesema litaharakisha Mchakato wa Uanzishwaji Sheria ya Bodi ya Usajili wa Wanajiosayansi nchini ikiwemo kuishauri Serikali na kueleza kuwa, ni fursa nzuri ya kusimamia rasilimali madini na itapunguza hasara kwa wadau. Kauli hiyo iliyotolewa Januari 23, jijini Dodoma na Makamu Mwenyekiti wa Kamati …

Soma zaidi »

MWADUI WAPEWA MWEZI MMOJA KUUZA ALMASI SOKO LA NDANI

Uongozi wa Mgodi wa Diamond Williamson (Mwadui) unaozalisha madini ya Almasi uliopo mkoani Shinyanga wilayani Kishapu umeagizwa na kupewa muda wa mwezi mmoja hadi kufikia Januari 2020 kuanza kuuza 5%  ya Almasi yote inayozalishwa katika mgodi huo kwenye soko la ndani hususani soko la Kishapu huku wazawa wakipewa fursa ya …

Soma zaidi »

NITAENDELEA KUONGEA KWA NAMBA (TAKWIMU) BADALA YA MANENO – WAZIRI WA MADINI DOTO BITEKO

Waziri wa Madini Doto Biteko amesema ataendelea kuongea kwa namba (takwimu) badala ya maneno huku akiongeza kuwa wizara yake itavuka malengo ya makadirio ya makusanyo ya fedha zilizopangiwa na wizara yake kukusanya ambayo ni bilioni 475 katika mwaka wa 2019/20 huku akibainisha kuuwa ndani ya miezi 5 tu teyari wizara …

Soma zaidi »