PROF KABUDI ZIARANI FALME ZA KIARABU

  • Tanzania na Nchi ya Falme za Kiarabu zimekubaliana kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi ikiwa ni pamoja na kushirikiana katika masuala ya usalama wa eneo la Ghuba na bahari ya Hindi pia kusaidia kuimarisha hali ya usalama katika nchi za Somalia na Sudan.
  • Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi alipomtembelea na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Umoja wa Falme za kiarabu Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan.
  • Katika Mazungumzo hayo wawili hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha udugu wa muda mrefu baina ya mataifa hayo mawili ikiwa ni pamoja na kufufua mazungumzo ya Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) ambayo kwa mara ya mwisho yalifanyika katika Mji wa Abu Dhabikatika Umoja wa Falme za Kiarabu ili kufufua na kutekeleza makubaliano ikiwa ni pamoja na kuangalia fursa za kiuchumi kwa faida ya pande zote mbili.
NJ
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi,akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Wizara ya Mambo ya Nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Abu Dhabi. June 30,2019.
  • Akizungumza mara baada ya mazungumzo hayo Waziri Palamgamba John Kabudi amesema pamoja na masuala mbalimbali waliyokubaliana pia Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Umoja wa Falme za kiarabu Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan ameahidi kufanya mazungumzo na Ubalozi wa Falme za Kiarabu uliopo Nchini Tanzania ili kuharakisha matayarisho ya Ubalozi huo kuhamia Dodoma baada ya serikali ya Tanzania kuupatia ubalozi huo eneo la kujenga ubalozi wa Nchi hiyo mjini Dodoma bure.
  • Waziri Kabudi ameongeza kuwa mazungumzo hayo yamekuwa ya manufaa kwa pande zote mbili na kwamba yataendelea kuimarisha mahusiano baina ya Nchi hizo mbili ikiwa ni pamoja na kufungua fursa za kibiashara kwa ajili ya maendeleo ya mataifa hayo.
  • Katika hatua nyingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof Palamagamba John Kabudi akizungumza wakati akihitimisha ziara yake Nchini China,amesema ziara hiyo imekuwa ya manufaa kiuchumi kwa Tanzania ambapo tayari wawekezaji takribani 150 wanatarajiwa kuwasili nchini Tanzania kwa nia ya kuangalia maeneo mbalimbali ya uwekezaji mapema mwezi septemba wakitanguliwa na ujumbe wa watu 10 mwezi Julai 2019,hii ikiwa ni kipindi kifupi sana mara baada ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuhudhuria mkutano wa kwanza wa maonesho ya uchumi na biashara kati ya China na Afrika uliofanyika katika mji wa Chanshang katika jimbo la Hunan,Nchini China.
NJ
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akisalimiana na mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Umoja wa Falme za kiarabu Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan,Abu Dhabi,Umoja wa Falme za Kiarabu. June 30,2019.
  • Aidha ametanabaisha kuwa tayari wamepatikana wawekezaji wanaotaka kujenga nyumba ya kulala wageni yenye vyumba mia tatu katika mji wa Karatu ulioko mkoani Manyara kwa nia ya kuhamasisha watalii hususani kutoka China ambao wanatarajiwa kuongezeka maradufu kufuatia hatua ya Tanzania kuweka msisitizo katika kutangaza vivutio vyake vya Utalii.
  • Pia Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Beijing kimekubali ombi la Waziri Kabudi la kutaka kuongeza idadi ya wanafunzi watakaokwenda kusoma chuoni hapo kutoka 20 hadi kufikia idadi 40 nafasi zitakazotolewa kwa ufadhili wa chuo hicho kila mwaka ili kuandaa nguvu kazi ya kutosha wakati Tanzania ikijiandaa kuingia katika uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.
Ad

Unaweza kuangalia pia

RAIS MAGUFULI AMTEUA BALOZI WILBERT IBUGE KUWA KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NJE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Balozi (Kanali) …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *