Imeelezwa kuwa, Dira ya Taifa ya Maendeleo ni picha na maono kuhusu mustakabali tarajiwa wa maendeleo ya nchi kwa siku za usoni.

Hayo yamebainishwa leo Julai 20, 2024 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko wakati akifungua Kongamano la Kwanza la Kikanda kuhusu Maandalizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 jijini Mwanza.

“Maandalizi ya Dira ni sehemu ya upangaji maendeleo na sisi kama Taifa ili tuweze kustawi hatuna budi kuchukua hatua madhubuti za kuchochea maendeleo ili kufikia kiwango tarajiwa katika siku za usoni.

Ad

Pia, kongamano ni sehemu ya zoezi la ushirikishaji wadau na ukusanyaji maoni ya Dira na makongamano kama hayo na mbinu nyingine zinazotumika kukusanya maoni ya wadau (mfano simu za mkononi, tovuti na mahojiano ya ana kwa ana katika ngazi ya kaya.

Ameongeza kuwa, kupitia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, Tanzania imeweza kupiga hatua kubwa ikiwemo kuingia kwenye orodha ya nchi ya uchumi wa kipato cha kati cha chini (lower middle-income country) mwaka 2020 baada ya kufikisha wastani wa kipato cha mtu cha dola za kimarekani 1,080.

“Ukiacha kipato na kiwango cha jumla cha maendeleo ya watu, Tanzania bado iko nyuma katika vipimo mbalimbali vya maendeleo ukilinganisha na viwango vya kimataifa pamoja na nchi nyingine zilizo katika kundi la uchumi wa kipato cha kati (middle-income countries),” ameongeza Dkt. Biteko.

Ad

Unaweza kuangalia pia

“Tukamate wajibu wetu tuliopewa na Mungu, wa Kukuza watoto wetu katika maadili mema”.‪@samiasuluhu99‬

Twende tukatunze Watoto wetu vile sisi tulivyotunzwa na Wazazi Wetu katika maadili mema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *