Waziri Mkuu

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo kuhakikisha inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuwawezesha mabondia kunufaika na vipaji vyao.

Ametoa Wito huo jana (Alhamisi, Desemba 26, 2024) wakati wa tukio maalum la pambano la ngumi la ‘Knockout ya Mama’ linalofanyika katika ukumbi wa Super Dome, Masaki jijini Dar es Salaam. “Awali michezo hii ilikuwa ni ridhaa, lakini kwasasa tumeweka sheria ambazo zinataka mchezo huu uwe wa kulipwa, ambayo mchezaji …

Soma zaidi »

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza kwa njia ya Simu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan alipopiga simu kuzungumza na wadau na Mashabiki wa mchezo wa ngumi, wakati wa tukio maalum la pambano la ngumi la ‘Knockout ya Mama’ linalofanyika katika ukumbi wa Super Dome, Masaki jijini Dar es Salaam, Desemba 26, 2024

Soma zaidi »

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa, ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Daraja la Sukuma lenye urefu wa mita 70 pamoja na barabara unganishi yenye urefu wa kilomita 2.3

Hafla hiyo ilifanyika katika mkoa wa Simiyu, ambapo Waziri Mkuu alisisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan ipo imara na imejidhatiti kuhakikisha huduma muhimu za kijamii zinawafikia wananchi wote nchini. Katika hotuba yake, Mheshimiwa Majaliwa aliwahakikishia wananchi kuwa Serikali itaendelea kufanya kazi …

Soma zaidi »

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Desemba 19, 2024 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kuaga mwili wa marehemu John Billy Tendwa ambaye aliwahi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini.

Akitoa Salama pole kwa waombolezaji wakati wa tukio la kuaga lililofanyika katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia ametoa wito kwa wanafamilia, ndugu na waombolezaji kuyaenzi mema yote aliyoyafanya marehemu Tendwa katika kipindi cha uhai wake. Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Marehemu Tendwa …

Soma zaidi »

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameviagiza vyombo vyote vya usalama vihakikishe watu wote waliokwama ndani ya jengo lililoporomoka katika kata ya Kariakoo jijini Dar es Salaam wanaokolewa huku mali zao zikilindwa.

Ametoa agizo hilo (Jumamosi, Novemba 16, 2024) baada ya kushuhudia juhudi za uokoaji zinavyoendelea baada ya jengo ghorofa nne kuporomoka katika eneo la Karikoo. Akizungumza baada ya kukagua juhudi za uokoaji katika eneo hilo kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Majaliwa amesema hadi sasa watu 40 mejeruhiwa ambapo …

Soma zaidi »

WAZIRI MKUU AONGOZA MAZIKO YA MAREHEMU LAWRENCE MAFURU

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Novemba 15, 2024 ameungana na ndugu, jamaa, marafiki na viongozi wengine wa Serikali katika mazishi ya aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Tume ya Mipango, Marehemu Lawrence Nyasebwa Mafuru. Maziko hayo yamefanyika katika Makaburi ya Kondo, Ununio jijini Dar es Salaam. Marehemu Mafuru alifariki Novemba 09, 2024 …

Soma zaidi »

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Marehemu Lawrence Mafuru kwenye viwanja vya Karimjee

Tukio la kuaga mwili wa Marehemu Lawrence Mafuru liliongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Soma zaidi »

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa Baraza la Mawaziri utasaidia kuboresha utendaji kazi na kuleta ufanisi zaidi katika kuwahudumia wananchi

Amesema kuwa maboresho hayo ya matumizi ya mfumo wa kielektroniki yatasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza matumizi ya karatasi katika vikao vya Serikali, hususan Baraza la Mawaziri, hivyo kupunguza changamoto ikiwemo kuchelewa kwa taarifa, gharama kubwa za uchapaji na hatari ya upotevu wa taarifa muhimu. Amesema hayo leo (Jumatatu, Novemba 11, …

Soma zaidi »

WAZIRI MKUU AMWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA KONGAMANO LA JUMUIYA YA WAISLAMU WA SHIA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Novemba 10, 2024 amemuwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano Mkuu na Kongamano la Umuhimu wa Amani kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Kongamano hilo linaloratibiwa na Jumuiya ya Waislamu wa SHIA Tanzania, lilofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini …

Soma zaidi »