TOFAUTI YA SENSA YA MWAKA 2022 NA SENSA ZILIZOPITA

Tofauti ya Sensa ya Mwaka 2022 na Sensa zilizopita:-
Katika sensa ya mwaka 2022 inatarajiwa kuwa na vitu vipya kama vile;
• Kutenga maeneo ya kijiografia ya kuhesabia watu katika ngazi za kitongoji/mtaa na upatikanaji wa taarifa za kitakwimu katika ngazi za kitongoji/mtaa pamoja na kuwa na mipaka ya kudumu katika ngazi hizo;
• Matumizi ya Vishikwambi (tablets) katika hatua zote za utekelezaji wa sensa kwa lengo la kupunguza gharama;
• Nyongeza ya maswali yatakayowezesha upatikanaji wa taarifa zaidi za kitakwimu ikilinganishwa na Sensa ya Mwaka 2012:-

  1. Taarifa za kidemografia (umri wakati wa ndoa ya kwanza);
  2. Maswali yanayohusu ulemavu (Kichwa kikubwa, Mgongo wazi, Kifafa/Epilepsy, Mbalanga/storiasis na Usonji/autism);
  3. Maswali ya uhamaji kulingana na mapendekezo ya IOM (International Organization of Migration);
  4. Maswali kuhusu umiliki wa nyaraka za kitaifa (vitambulisho NIDA, vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo wadogo, Mzanzibari mkazi, hati ya kusafiria, na leseni ya udereva);
  5. Maboresho ya maswali ya shughuli za kiuchumi ikiwa ni pamoja na idadi ya kaya ziliko kwenye sekta isiyo rasmi;
  6. Umiliki wa ardhi na taarifa za TEHAMA
    • Takwimu za nyumba (orodha, hali ya umiliki na aina ya nyumba)
    • Maswali ya kilimo na mifugo

MatokeoChayA+

Ad

Unaweza kuangalia pia

#LIVEDAY2: JUKWAA LA KODI NA UWEKEZAJI 2024

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.