Ni vigumu ukishasifiwa maeneo mengine yote halafu ukakuta eneo unalolisimamia usisifiwe – Rais Magufuli

Nukuu za Rais Dkt. John Magufuli katika Kikao kilichowakutanisha viongozi Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Wakuu wa Mikoa, Mawaziri na Makatibu Wakuu wa baadhi ya Wizara.

  • “Na saa nyingine huwa ni vigumu ukishasifiwa maeneo mengine yote halafu ukakuta eneo unalolisimamia usisifiwe, huwa linavunja moyo. Lakini ni vyema niwaeleze ukweli na nitatoa takwimu nikilinganisha na nchi nyingine”:-
  • “Ukilinganisha labda na nchi zilizoko ndani ya Afrika.. nchi ya Tanzania yenye idadi ya watu karibu milioni 54-55, idadi ya walipa kodi ukiacha  hizi juhudi ambazo zimezungumzwa sasa, ilikuwa ni watu 2,273,153! 2,273,153… katika nchi yenye idadi ya watu milioni karibu mil. 54-55! Uwiano wa kodi wa GDP kwa % tuna 12.8;
  • Ukienda Kenya, ina idadi ya watu mil 46,600,000 idadi ya walipa  kodi ni 3,940,000. Uwiano wa kodi kwa GDP kwa % ni 18.5%. Sisi tuko 12.8% ; Kenya ambao ni wachache zaidi.. sisi tuko mil 55 wao mil. 46, wako 18.5%! Rwanda; Idadi ya watu Rwanda ni 11,671,371. Walipakodi ni 172,422. Uwiano wa kodi kwa GDP ni 15.8%. Uganda; Idadi ya watu 37,746,217. Walipakodi ni  1,320,621. Uwiano wa kodi kwa GDP ni 14.2%.
RAIS AKIZUNGUMZA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizingumza na Wakuu wa Mikoa, Mawaziri na Makatibu Wakuu wa baadhi ya Wizara, Mameneja wa Mikoa wa Mamlaka ya Mapato nchini TRA, Waakilishi wa Machinga kabla ya kutoa Vitambulisho kwa ajili ya Wafanyabiashara wadogo wadogo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Vitambulisho hivyo vitagharimu kiasi cha Shilingi 20,000/ kwa kila kimoja.
  • Burundi; Idadi ya wananchi wa Burundi ni 10,400,938. Idadi ya walipa kodi 22,591. Uwiano kwa kodi kwa GDP ni 13%. Afrika ya Kusini; Idadi ya wananchi ni 56,522,000. Walipakodi wao ni 19,980,110. Uwiano wa kodi kwa GDP ni 26%. Sisi 12.8%.. Afrika ya kusini ambayo idadi ya population Inakaribiana karibiana, wao ni 26%! Botswana; Idadi ya watu wa nchi ya Botswana ni 2,254,021. Walipakodi wao ni 734,470. Uwiano wa kodi kwa GDP ni 14%. Zambia; Wako 16,405,229. Walipakodi ni 872,748. Uwiano wa kodi kwa GDP 15.8%. Msumbiji; Wako 27,128,530. Walioakodi wa Msumbiji ni 5,321,669!. Wako mil.27.1, walipakodi ni mil.5.3! Uwiano wa kodi kwa GDP ni 18%.
  • Namibia; Wako milioni 2.3 Walioakodi wao ni 666,763! Ni almost moja ya Tatu ya Wanamibia wanalipa kodi! Uwiano uko 12%Unapoangalia takwimu hii, ndipo sisi wakusanya Kodi na Wizara ya fedha ndipo mahali panapotakiwa kuanza kujiuliza!..”- Rais Dkt. John Magufuli. Dec 10,2018

 

 

Ad

Unaweza kuangalia pia

LIVE: UZINDUZI WA MAJENGO YA OFISI YA MANISPAA NA MKUU WA WILAYA KIGAMBONI JIJINI DSM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 11, Febuari, …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *