KIKAO CHA MAWAZIRI KUHUSU BOMBA LA MAFUTA KUFANYIKA KAMPALA WIKI IJAYO

  • Kikao cha Tatu (3) cha mawaziri wa sekta zinazohusika na utekelezaji wa mradi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), kinatarajiwa kufanyika Januari 25, 2019 jijini Kampala.
sehemu ya jambo
Sehemu ya wajumbe wa kikao cha maandalizi kwa timu ya Tanzania inayotekeleza Mradi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP); kabla ya kwenda Uganda kushiriki kikao cha majadiliano na Timu ya nchi hiyo, Januari 25, mwaka huu. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Wizara ya Nishati, Dodoma
  • Kikao hicho kitakachotanguliwa na vikao ngazi ya wataalamu na baadaye ngazi ya makatibu wakuu wa Wizara husika, kitaongozwa na Mawaziri wenye dhamana ya nishati, ambao ni Dkt. Medard Kalemani (Tanzania) na Mhandisi Irene Muloni (Uganda).
  • Akizungumza Wizara ya Nishati jijini Dodoma, wakati wa kikao cha maandalizi kilichoshirikisha timu ya Tanzania inayohusika na usimamiaji wa utekelezaji wa mradi husika; Waziri Kalemani alitoa rai kwa wajumbe wote kufanya kazi kwa ushirikiano, kujituma na weledi wa hali ya juu ili kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kwa wakati kwa faida ya Taifa.
SHE
Sehemu ya wajumbe wa kikao cha maandalizi kwa timu ya Tanzania inayotekeleza Mradi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP); kabla ya kwenda Uganda kushiriki kikao cha majadiliano na Timu ya nchi hiyo, Januari 25, mwaka huu. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Wizara ya Nishati, Dodoma
  • Kwa upande wake, Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Paramagamba Kabudi, amesema anayo imani kubwa na kila mjumbe wa timu husika kwamba kuteuliwa kwao kuwa sehemu ya timu hiyo kumetokana na sifa zao kiutendaji na utaalamu, hivyo akawataka kutomwangusha Rais John Magufuli na Taifa kwa ujumla katika kutekeleza jukumu walilopewa.
Waziri wa Katiba na Sheria,
Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Paramagamba Kabudi, akifafanua jambo wakati wa kikao cha maandalizi kwa timu ya Tanzania inayotekeleza Mradi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP); (hawapo pichani) kabla ya kwenda Uganda kushiriki kikao cha majadiliano na Timu ya nchi hiyo, Januari 25, mwaka huu. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Wizara ya Nishati, Dodoma
  • Naye Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Adelardus Kilangi, akichangia mjadala katika kikao hicho, alisema Ofisi yake imejipanga kutoa ushauri wote wa kisheria katika kuhakikisha mikataba mbalimbali inayoingiwa baina ya Tanzania na Uganda katika utekezaji wa mradi husika, inafuata misingi yote ya kisheria kwa manufaa ya Taifa.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kushoto) na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano na Mazingira, Mussa Sima wakifuatilia mjadala wakati wa kikao cha maandalizi kwa timu ya Tanzania inayotekeleza Mradi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP); (hawapo pichani) kabla ya kwenda Uganda kushiriki kikao cha majadiliano na Timu ya nchi hiyo, Januari 25, mwaka huu. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Wizara ya Nishati, Dodoma
  • Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanznia na Serikali ya Jamhuri ya Uganda zilisaini Mkataba wa makubaliano, Mei 26, 2017 ambao umeweka misingi ya utekelzaji wa mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).
Kutoka kulia ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Adelardus Kilangi,
Kutoka kulia ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Adelardus Kilangi, Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani na Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Paramagamba Kabudi, wakifuatilia mjadala wakati wa kikao cha maandalizi kwa timu ya Tanzania inayotekeleza Mradi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP); (hawapo pichani) kabla ya kwenda Uganda kushiriki kikao cha majadiliano na Timu ya nchi hiyo, Januari 25, mwaka huu. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Wizara ya Nishati, Dodoma
  • Tangu kusainiwa mkataba huo, Timu ya Majadiliano ya Serikali (GNT) imefanya vikao mbalimbali vya majadiliano na Timu ya Uganda katika miji ya Dar es Salaam na Arusha (Tanzania) pamoja na Kampala Uganda.
Ad

Unaweza kuangalia pia

SERIKALI KUTOINGILIA TAALUMA YA UKAGUZI WA HESABU ZA FEDHA

Serikali imeeleza kuwa haina mpango wa kuingilia taaluma ya ukaguzi wa hesabu nchini kwa kuondoa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *