- Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai (Mb) leo azindua Jengo la kisasa lililojengwa kwa kutumia teknologia ya moladi Wilayani Kondoa
- Akiwa mgeni Rasmi katika uzinduzi wa Mahakama ya Wilaya ya Kondoa alisema miundo mbinu bora na ya kisasa katika muhimili wa Mahakama inawezesha mazingira tulivu ya uwekezaji na ukuaji wa biashara na hivyo kukuza Uchumi wa mtanzania na Taifa kwa ujumla wake.
- Aidha, alisema anafarijika kwa niaba ya wanadodoma wote kuona upatikanaji wa majengo ya kisasa ya Mahakama kuanzia ngazi za mahakama za mwanzo hadi Wilayani.
- Pia, Mhe. Spika alisema Mifumo ya TEHAMA katika Mahaka ya kisasa kama hii itaboresha utoaji wa huduma za kimahakama na uharakishaji wa utoaji haki kwa wakati na kwa wote, aliwaomba Wananchi kutoa ushirikiano na chombo cha Mahakama kalinda na kutunza rasilima hiyo ya jengo kwani zimetumika fedha za ndani ambayo ni kodi za Wananchi.
- Ili kutimiza adhima ya Mahakama Mh.Job aliahidi kutoa ushirikiano wa hali na mali katika kupitisha Bajeti zinazowasilishwa na Mahakama Bungeni ili kutoa fursa za kuendelea kuboresha Miundo mbinu ya Mahakama nchini alikiri kuwa takribani nchi nzima majengo ya mahakama ni mabovu na yaliyochakaa sana.
Ad