SERIKALI IMERIDHIA OMBI LA WAKAZI WA MAGOMENI KOTA KUNUNUA NYUMBA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Msanifu majengo Daud Kondoro wakati alipokuwa akitoa maelezo kuhusu hatua mbalimbali za Ujenzi wa Nyumba 644 katika eneo la Magomeni Kota Mkoani Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akikabidhi mfano wa Ufunguo kwa Bibi Mwajuma Sama na Mzee Henry Ngwemba kwa ajili ya kuwakabidhi Nyumba mara baada ya kuzindua rasmi mradi wa Nyumba 644 Magomeni Kota Mkoani Dar es Salaam leo tarehe 23 Machi 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akikagua mradi wa Nyumba 644 zilizojengwa na Serikali kupitia Wakala wa Majengo Tanzania TBA katika eneo la Magomeni Kota Mkoani Dar es Salaam leo tarehe 23 Machi, 2022
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Mkoa wa Dar Es salaam baada ya kuzindua mradi wa Nyumba 644 zilizojengwa na Serikali kupitia Wakala wa Majengo Tanzania TBA katika eneo la Magomeni Kota Mkoani Dar es Salaam leo tarehe 23 Machi, 2022.
Sehemu ya Wananchi pamoja na Wakazi wa Magomeni Kota Mkoani Dar es Salaam wakihudhuria Sherehe za uzinduzi wa Nyumba 644.

Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameridhia ombi la wakazi wa Magomeni Kota la kununua nyumba zilizojengwa na Serikali kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA,) katika eneo hilo kwa kutoa maelekezo kwa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kuruhusu wakazi hao kununua nyumba hizo kwa utaratibu wa Mpangaji-Mnunuzi kwa kurejesha fedha ya ujenzi pekee bila gharama ya ardhi.


Rais Samia ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akizindua nyumba 644 zilizopo katika eneo la Magomeni Kota na kueleza kuwa kama ilivyoahidiwa na mtangulizi wake Hayati Dkt. John Joseph Magufuli  wakazi hao wataishi miaka mitano bure na kwa miezi mitatu ya awali hawatachangangia gharama za huduma jumuishi.

Ad
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Africa50, Alain Ebobisse aliyeambatana na Ujumbe wake Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 23 Machi, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Africa50, Alain Ebobisse aliyeambatana na Ujumbe wake Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 23 Machi, 2022.


”Nimeridha kuwa baada ya miaka mitano wananchi wa Magomeni Kota kuuziwa nyumba hizi kwa utaratibu wa  Mpangajii-Mnunuzi na kurejesha gharama za ujenzi pekee, hatutawatoza gharama ya ardhi kwa sababu tukifanya hivyo mtashindwa kuzinunua.” Amesema.


Aidha amesema, kwa wakazi ambao wapo tayari kulipa gharama za ununuzi wa nyumba hizo wanaruhusiwa kulipa kidogo kidogo bila riba huku wakiendelea kuishi katika makazi hayo.
Kuhusiana na utunzaji wa mradi huo Rais Samia amewataka wakazi hao kuzingatia usafi na kudumisha upendo na mshikamano


”Ninawaomba mtunze mradi huu kwa kuzingatia usafi wa nyumba hizi ambao ni dhamana yenu kwa sasa, nyumba kama hizi tunategemea mpikie gesi hatutegemei mpikie kuni katika maghorofa haya.” Amesema.

Ad

Unaweza kuangalia pia

Serikali ya Tanzania na Czech Zakubaliana Kuondoa Utozaji Kodi Mara Mbili

Serikali za Tanzania na Czech kukuza ushirikiano wa kiuchumi na kuvutia uwekezaji kati yao. Kuondoa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *