Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiizindua Barabara ya Kilomita Tatu ya Wawi – Mabaoni – Mgogoni ikiwa ni shamra shamra za Mapinduzi ya Zanzibar kutimia Miaka 55.

BALOZI SEIF AZINDUA BARABARA CHAKE CHAKE PEMBA

  • Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewakumbusha Wananchi wanaoishi pembezoni mwa Miundombinu ya Barabara Nchini kuwa walinzi kwa kutoa Taarifa kwa vyombo husika dhidi ya wale wanaoharibu kwa makusudi miundombinu hiyo iliyojengwa kwa gharama kubwa.
    Muonekano wa Barabara
    Muonekano wa Barabara ya Wawi Mabaoni – Mgogoni iliyozinduliwa na Balozi Seif imeigharimu Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zaidi ya Shilingi Bilioni 1.9.
  • Alisema wapo baadhi ya Watu waliojitoa mshipa wa fahamu kwa kuiba alama zilizowekwa Bara barani, kuchimba Mchanga au udongo pembezoni mwake jambo ambalo kama Wananchi hawatakuwa tayari kutoa ushirikiano wao kwa vyombo vya Dola  ile azma ya Serikali ya kuimarisha Sekta ya Mawasiliano inaweza kufifia.
    Balozi Seif akiikagua Bara bara
    Balozi Seif akiikagua Bara bara Mpya ya Wawi hadi Mgogoni iliyojengwa na Kampuni ya Mecco akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar Nd. Mustaha Aboud Jumbe.
  • Balozi Seif Ali Iddi alitoa kumbusho hilo wakati wa hafla ya kuizindua rasmi barabara ya Kilomita Tatu iliyojengwa kwa Kiwango cha Lami kuanzia Wawi -Mabaoni  hadi Mgogoni Chake Chake Pemba ikiwa ni mwanzoni mwa Shamra shamra za Maadhimisho ya kusherehekea Miaka 55 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
     Balozi Seif akimpongeza Mwakilishi
    Balozi Seif akimpongeza Mwakilishi wa Kampuni ya Ujenzi ya Mecco Bwana Bujet kutokana na Wahandisi wake kukamilisha ujenzi wa Bara bara ya Wawi – Magogoni kabla ya wakati uliokubalika ndani ya Mkataba.
  • Alisema uzoefu unaonyesha wazi kwamba mahala popote palipojengwa Miundombinu ya Bara bara katika kipindi kifupi hutoa fursa kwa Wananchi wake kuimarika Kiuchumi kutokana na harakati za Kibiashara zinazoambatana na ujenzi wa Makaazi bora yanayolingana na uwepo wa Bara bara husika.
    ZENJI-1
    Balozi Seif akizungumza na Wananchi wa Wilayua ya Chake chake katika hafla ya uzinduzi wa Barabara ya Wawi – Mabaoni – Mgogoni ndani ya shamra shamra za maadhimisho ya Sherehza kutimia Miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Ad

Unaweza kuangalia pia

RAIS MAGUFULI ATEMBELEA DAR ES SALAAM ZOO, AVUTIWA NA WANYAMA WENGI WANAOFUGWA HUMO

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *