Waziri wa Madini, Doto Biteko akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Uranium One Holdings N.V, Vladimir Hlavinka mara baada ya kuwasili ofisini kwake kwa mazungumzo. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mantra, Fredrick Kibodya.

MRADI WA MADINI YA URANIUM UNATARAJIWA KULIINGIZIA TAIFA KODI YA DOLA MILIONI 220 KWA MWAKA

Waziri wa Madini, Doto Biteko
Waziri wa Madini, Doto Biteko akimsikiliza Makamu wa Rais wa kampuni ya Uranium One Holdings N.V, Vladimir Hlavinka akielezea nia yao ya kutaka kuwekeza katika sekta ya madini nchini wakisubiri uwekezaji wao katika masuala ya uranium uliositishwa kwa muda.
  • Uwekezaji uliofanyiwa katika mradi wa uchimbaji madini ya uranium katika mto Mkuju ulioko mkoani Lindi ya Uranium One umefikia kiasi cha dola za kimarekani Milioni mia mbili ($200mil) toka mradi ulipoanza mwaka 2009.
  • Akizungumzia na Waziri wa Madini Dotto Biteko mjini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Uranium One, Frederick Kibodya amesema manufaa ya mradi huo ni pamoja na kusaidia katika kukuza teknolojia nchini. Amesema madini hayo yakichimbwa yanatumika katika kuzalisha umeme ambayo ni teknolijia mpya nchini.
  • Aidh Mkurungezi huyo amesema kuwa mradi utasaidia katika kuongeza ajira nchini na  kufafanua kuwa kwa kipindi cha ujenzi wa mradi wanatarajia kuajiri watanzania 1600 kwa kipindi cha miezi kumi na nane.
  • Aidha, alibainisha kuwa kutakuwepo na uzalishaji kwaajila sekta  zisiso rasmi kiasi cha watu 4500 wakati wa ujenzi na 2300 pindi uzalishaji utakapoanza.
  • Pia Kibodya amesema, mradi unatarajia kuliingizia taifa pato la kiasi cha dola za kimarekani milioni 220 kama kodi kwa mwaka, kiasi ambacho kitakuwa kikibadilika kadri uzalishaji unavyoongezeka.
  • Mradi wa uchimbaji madini ya uranium katika mto Mkuju unafanywa kwa ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania na Mbia wa kampuni ya Mantra anayejulikana kama Rosatom.

Ad

Unaweza kuangalia pia

SOKO LA MDINI ULANGA LA KUSANYA MILIONI 396 NDANI YA MIEZI 5

Waziri wa Madini Doto Biteko amesema tangu kuanzishwa kwa soko la madini Ulanga wamenunua madini …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *