JOSHUA NASSARI AONGOZA WAWEKEZAJI TOKA CHINA KUANGALIA FURSA TANZANIA

2-01
Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Bw.Geoffrey Mwambe (mwenye tai nyekundu) akizungumza Wawekezaji kutoka Jimbo la Hebei Nchini China waliotembelea ifisi za TIC Jumatano Desemba 11, kushoto kwake ni Maafisa wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC.(Picha na Latiffa Kigoda)
  • Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arumeru Joshua Nassari leo tarehe 11 Desemba,2019 ameongoza kundi la wafanyabiashara  wapatao kumi kufika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).
  • Wageni hao wamefika kutoka jimbo la  Hebei, China ambao  wameonesha nia ya kuwekeza nchini kwenye miradi mbalimbali ya kuanzisha. Viwanda hivyo ni pamoja na kiwanda cha kuunganisha magari, kiwanda cha kutengeneza vioo vya milango na madirisha na kiwanda cha kutengeneza chakula.
3-01
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC Bw. Geoffrey Mwambe akiwa katika Picha ya Pamoja na Wawekezaji kutoka Jimbo la Hebei Nchini China pamoja na Maafisa wa Kituo hicho, Wawekezaji hao walitembelea ofisi za TIC Jumatano Desemba 11 wakiongozwa na aliyekuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari (wa pili kutoka kulia mwenye shati na tai). Picha na Latiffa Kigoda.
  • Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Geoffrey Mwambe amewakaribisha na kuwahakikishia utayari wa Serikali kuwasaidia kupata ardhi, vibali, leseni na vyeti vinavyotakiwa ili kufanikisha mipango yao ya uwekezaji nchini.
  • TIC ipo mstari wa mbele katika kuhamasisha, kuvutia na kusaidia wawekezaji wazawa na wageni kwa kuwa utekelezaji wa miradi hiyo, una matokeo makubwa yenye manufaa kwa Taifa na wananchi ikiwamo uzalishaji wa ajira.
Ad

Unaweza kuangalia pia

WAZIRI KAIRUKI AWAHAKIKISHIA WAWEKEZAJI MAZINGIRA MAZURI YA UWEKEZAJI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Uwekezaji nchini Mhe. Angellah Kairuki …

Oni moja

  1. Big up
    Maendeleo hayana chama

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.