DKT. KIJAJI AKUTANA NA WAKUU WA TAASISI BAADA YA WIKI TATU TANGU KUAPISHWA KWAKE

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Zainab Chaula akizungumza wakati wa kikao kazi cha Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Ashatu Kikaji (kushoto) na wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo (hawapo pichani) katika ukumbi wa Ofisi za Wizara hiyo zilizopo mji wa Serikali Mtumba, Dodoma

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Ashatu Kijaji amekutana na Wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara katika kikao kazi kilichofanyika jana tarehe 04/10/2021 katika ofisi za Wizara hiyo zilizopo mji wa Serikali Mtumba, Dodoma baada ya wiki tatu tangu alipoteuliwa na kuapishwa kuongoza Wizara hiyo

Dkt. Kijaji amesema kuwa kikao hicho kilikuwa na lengo la kufahamiana, kukumbushana na kutambua majukumu yao katika Taifa kwa kuitumikia Serikali iliyopo madarakani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambayo iliingia Mkataba mahsusi na wananchi kupitia Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 – 2025

Ad

“Wizara hii ni sehemu ya Serikali na tuna jukumu la kuhakikisha Mkataba ambao chama cha CCM kiliingia na wananchi unatekelezeka ipasavyo katika tasnia za Habari, Mawasiliano na TEHAMA kwa kutekeleza jukumu kubwa la kuwawezesha watanzania kupata mawasiliano na habari ambazo zina athari chanya kwenye maisha yao kijamii na kiuchumi”, amezengumza Dkt. Kijaji

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Kundo Mathew akizungumza wakati wa kikao kazi cha Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Ashatu Kikaji (katikati) na wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo katika ukumbi wa Ofisi za Wizara hiyo zilizopo mji wa Serikali Mtumba, Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula.

Amesema kuwa Wizara hiyo ni Wizara wezeshi lakini imekuwa ikichangia pato la Taifa kwa asilimia 1.5 kwa miaka minne mfululizo kitu ambacho anakiona hakijakaa sawa hasa ukizingatia kama Taifa tunaelekea kwenye uchumi wa dijitali ambapo Wizara hiyo pamoja na taasisi zake wanapaswa kuangalia upya na kuleta mabadiliko ya mchango wao kwa pato la Taifa

Ameongeza kuwa watendaji wakuu wa taasisi za Wizara yake wahakikishe wanakuwa wazalendo na kuleta tafsiri sahihi ya viti walivyoaminiwa na Serikali kuvikalia kwa kuhakikisha wanawafikishia watanzania huduma zenye viwango na ubora unaohitajika

Kwa upande wa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula amezungumzia kikao hicho kuwa kilikuwa ni kikao cha Waziri kufahamiana na Wakuu wa taasisi na kukumbushana kutimiza wajibu kwa watendaji hao kuwajibika kwa matokeo ambayo ni kutoa huduma bora kwa wananchi na kuhakikisha taarifa za utekelezaji wa matokeo chanya zinamfikia mwananchi

Kaimu Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Tuma Abdallah akizungumza wakati wa kikao kazi cha Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Ashatu Kikaji (hayupo pichani) na wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo katika ukumbi wa Ofisi za Wizara hiyo zilizopo mji wa Serikali Mtumba, Dodoma

Naye Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Macrise Mbodo amesema kuwa kikao hicho kimetengeneza uelewa wa pamoja kati ya utendaji wa taasisi na matamanio na matarajio ya Waziri huyo ya utendaji wa taasisi hizo kwa matokeo ambapo wakuu wa taasisi hizo walipata fursa ya kueleza majukumu ya msingi ya taasisi zao, zilipotoka na zinapoelekea

Kikao hicho kilihudhuriwa na wakuu wa taasisi za Wizara hizo ambazo ni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Shirika la Posta Tanzania (TPC), Tume ya TEHAMA (ICTC) na Baraza la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano (TCRA-CCC).

Ad

Unaweza kuangalia pia

Mitazamo ya Uongozi ya Mhe. Ummy Ally Mwalimu katika Sekta za Afya, Maendeleo ya Jamii, na Haki za Watoto

Ummy Ally Mwalimu ameonyesha mitazamo ya uongozi yenye mwelekeo wa kujali maendeleo na ustawi katika …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *