Maktaba Kiungo: WIZARA YA NISHATI

NAIBU WAZIRI NISHATI ATAKA BUSARA ITUMIKE KUUNGANISHA UMEME VIJIJINI

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini kutumia busara katika kazi hiyo ili iwaongoze kufanya maamuzi sahihi hususan uunganishaji umeme katika taasisi na miradi ya umma. Alitoa wito huo kwa nyakati tofauti jana, Februari 25 mwaka huu, akiwa katika ziara ya kazi wilayani Nachingwea, …

Soma zaidi »

NAIBU WAZIRI NISHATI AKERWA NA MKANDARASI MBABAISHAJI

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amekemea vikali utendaji kazi mbovu wa Mkandarasi State Grid, anayetekeleza mradi wa umeme vijijini Mkoa wa Lindi, kutokana na kufanya kazi chini ya kiwango na kutokamilisha wigo wake kwa wakati kama mkataba unavyoelekeza. Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nangambi Naipuli, Kata ya Mingumbi, …

Soma zaidi »

NCHI ZA MASHARIKI MWA AFRIKA ZA DHAMIRIA KUIMARISHA UCHUMI KWA KUUZIANA UMEME

Nchi zilizopo Mashariki mwa Afrika, zimedhamiria kwa nia moja kuimarisha uchumi wao kwa kuuziana umeme kupitia mifumo ya kusafirisha nishati hiyo, iliyounganishwa katika ukanda husika. Hayo yalibainishwa Februari 21 mwaka huu, katika Mkutano wa 14 wa Baraza la Mawaziri wanaohusika na umeme kutoka nchi za ukanda huo, ambazo zimeunganishiwa mifumo …

Soma zaidi »

WACHIMBAJI WADOGO WILAYANI MBOGWE KUPATA UMEME NDANI YA SIKU KUMI

Wachimbaji wadogo katika machimbo ya Nyakafuru yaliyo katika Kijiji cha Nyakafuru wilayani Mbogwe wameonesha kufurahishwa na ahadi ya Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani ya kufikisha umeme katika machimbo hayo ndani ya siku kumi. Ahadi hiyo aliitoa jana mara baada ya kufanya ziara ya kikazi wilayani Mbogwe mkoani Geita ambapo …

Soma zaidi »

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 26 KUHUSU MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME

Kamishana wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga, kutoka Wizara ya Nishati, ameongoza timu ya wataalamu wa nishati kutoka Tanzania, kushiriki katika mkutano wa 26 wa Kamati Tendaji unaojadili mifumo ya kusafirisha umeme, iliyounganishwa katika nchi zilizopo Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool – EAPP) Mkutano huo unaofanyika, …

Soma zaidi »

KAZI YA UWASHAJI UMEME VIJIJINI INAZIDI KUSHIKA KASI – DKT. KALEMANI

Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani, ameeleza kuwa kasi ya usambazaji umeme vijijini inaendelea kuongezeka ili kuweza kufikia lengo la Serikali la kusambazia umeme vijiji vyote ifikapo mwaka 2021. Dkt. Kalemani aliyasema hayo jana akiwa katika ziara ya kukagua kazi ya usambazaji umeme katika Wilaya ya Geita mkoani Geita ambapo …

Soma zaidi »

NAIBU WAZIRI NISHATI AWATAKA WANA-PWANI WACHANGAMKIE UMEME WA REA

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu ametoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Pwani, hususan wanaopitiwa na Mradi wa Umeme Vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kuchangamkia fursa hiyo kutokana na unafuu wa gharama zake. Alitoa rai hiyo kwa nyakati tofauti akiwa katika ziara ya kazi kukagua utekelezaji wa …

Soma zaidi »

RAIS MAGUFULI AMETIMIZA NDOTO YA BABA WA TAIFA – MCHENGERWA

Serikali imekabidhi rasmi eneo la mradi wa umeme wa maporomoko ya maji ya Mto Rufiji (RHPP), kwa mkandarasi Kampuni ya Arab Contractors kwa pamoja na ile ya Elsewedy  Electric zote kutoka nchini Misri.  Hatua hiyo sasa inaashiria kuanza kwa kazi ya ujenzi wa mradi huo wa umeme ambao utazalisha Megawati …

Soma zaidi »

WAFANYABIASHARA WA MAFUTA KUJIUNGA KATIKA UMOJA WA KISEKTA NI HIARI SIYO LAZIMA – KALEMANI

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amesema kamwe Serikali haiwezi kumlazimisha mdau yeyote wa sekta ya mafuta nchini kujiunga na Chama, Jumuiya au Umoja wowote wa kisekta kwani hilo ni suala la hiyari kwa kila mmoja. Badala yake, Waziri Kalemani, ameushauri uongozi wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Mafuta Tanzania (Tanzania …

Soma zaidi »

WANANCHI WA IGANDO WAANZA KUPATA HUDUMA YA UMEME

Wananchi katika Kijiji cha Igando, wilayani Chato, mkoa wa Geita, wameanza kupata huduma ya umeme kupitia mradi wa Usambazaji Umeme Vijijini wa Awamu ya Tatu (REAIII) unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Waziri wa Nishati, Dkt  Medard   Kalemani ndiye aliyewasha rasmi umeme  katika …

Soma zaidi »