Maktaba ya Mwezi: November 2019

DKT KALEMANI ATAKA TANESCO IFANYE KAZI KAMA KAMPUNI ZA SIMU

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amewaagiza mameneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuwafuata wamiliki wa viwanda, migodi ya madini na hoteli kuwashawishi watumie umeme ili kuzalisha kwa tija hali itakayolipatia shirika hilo mapato zaidi kutokana na malipo ya umeme. Akizungumza na Kamati ya Ulinzi na Usalama ofisini kwa …

Soma zaidi »

STAMICO HII HAIWEZI KUFUTWA – KAMATI YA BUNGE

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mashirika ya Umma imesema Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) haliwezi kufutwa tena kutokana na mwenendo wa sasa kuridhisha kutokana na utendaji wake na kubadili mtazamo wa awali. Kubadili kwa mtazamo huo kunatokana na mwenendo wa awali kutoridhisha katika utendaji wake hali iliyopelekea baadhi …

Soma zaidi »

BODI YA REA YAMPA SIKU 14 MKANDARASI WA UMEME MKOANI SIMIYU KUJIREKEBISHA

Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imempa siku 14 mkandarasi wa umeme vijijini mkoani Simiyu kuongeza kasi ya usambazaji umeme katika vijiji alivyopangiwa la sivyo Bodi hiyo haitasita kuchukua hatua mbalimbali za kimkataba ikiwemo ya kusitisha mkataba. Mwenyekiti wa Bodi ya REA, Wakili Julius Kalolo  alisema hayo tarehe 16 …

Soma zaidi »

MKANDARASI WA UMEME WILAYANI CHATO ATEKELEZA MAAGIZO YA BODI YA REA

Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeeleza kuridhishwa kwake na utekelezaji wa maagizo iliyoyatoa kwa Mkandarasi anayefanya kazi ya kusambaza umeme vijijini wilayani Chato kampuni ya Whitecity Guangdong JV ambayo yalilenga kuongeza kasi ya usambazaji umeme vijijini. Hayo yalielezwa na Mwenyekiti wa Bodi ya REA, Wakili Julius Kalolo tarehe …

Soma zaidi »

KAMPENI YA ELIMU KWA MLIPAKODI YAWAFIKIA WAFANYABIASHARA ZAIDI YA 700 MOROGORO

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewafikia na kuwaelimisha wafanyabiashara zaidi ya 700 kupitia kampeni ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi iliyofanyika mkoani Morogoro. Lengo la kampeni hiyo ilikuwa ni kutoa elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kodi pamoja na kusikiliza malalamiko, changamoto na maoni kutoka kwa wafanyabiashara hao. Akizungumza mara baada …

Soma zaidi »

WATUMISHI FANYENI KAZI KWA UADILIFU, UTIIFU NA WELEDI – SHIGELA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigela amewataka watumishi wa Umma kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya utumishi, Uadilifu, utiifu, weledi, taratibu na sheria za kazi katika kutumiza majukumu yao kila siku. Shigela alisema hayo, Novemba 14, 2019 kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Utumishi, Dkt. Laurian Ndumbaro, …

Soma zaidi »

TANZANIA NA ANGOLA ZAJADILI USHIRIKIANO KATIKA MAFUTA NA GESI

Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani amekutana na Balozi wa Angola nchini Tanzania, Sandro De Oliveira na kufanya mazungumzo kuhusu  ushirikiano katika utafiti wa Mafuta na Gesi pamoja na ununuzi wa mafuta. Mazungumzo kuhusu ushirikiano huo yalifanyika tarehe 14/11/2019 jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Kaimu Kamishna wa Petroli na Gesi, …

Soma zaidi »