NAIBU WAZIRI SIMA – MIFUKO MBADALA ISIYOKIDHI VIWANGO MARUFUKU NCHINI

  • Serikali imesema kamwe haitaruhusu uzalishaji, uingizaji na matumizi ya mifuko mbadala aina ya Non-Woven isiyokidhi viwango vya 70 Gram Per Square Metre (GSM) kutumika nchini.
  • Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mussa Sima katika Mkutano wa Mashauriano baina ya Serikali, Wafanyabiashara na Wawekezaji uliolenga  kusikiliza na kutatua changamoto zao, Mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Uuguzi Kibaha mkoa wa Pwani.
  • Awali akiwasilisha taarifa ya Mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo amesema kuwa kumekuwa na uchelewashaji wa utoaji wa vibali vya kuingiza mifuko mbadala nchini kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira hali ambayo inaleta vikwazo kwa wafanyabiashara na wawekezaji.
22-01
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima akitoa ufafanuzi wa hoja zilizojitokeza katika Mkutano  wa Mashauriano baina ya Serikali, Wafanyabiashra na Wawekezaji katika ukumbi wa Chuo cha Wauguzi Kibaha Pwani.
  • Akitoa ufafanuzi wa ucheleweshaji wa vibali hivyo Mhe. Sima amesema kuwa Serikali imepiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki nchini tangu Juni Mosi 2019 na kutoa fursa kwa wakezaji kuagiza na kuzalisha mifuko mbadala ili kukidhi soko la ndani.
  • Hata hivyo changamoto imejitokeza kwa wafanyabiashara wasio waaminifu kutaka kuingiza mifuko isiyokidhi viwango aina ya Non-Woven. “Kumeanza kujitokeza uvunjifu wa sheria katika uzalishaji na uingizaji wa mifuko mbadala aina ya non-woven. Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeweka vigezo vya mifuko mbadala aina ya non-woven inayoweza kutumika nchini ikiwa ni pamoja na Uzito usiopungua GSM 70 (Gram per Square Metre), iweze kurejelezwa, Ioneshe uwezo wa kubeba, anuani ya mzalishaji na iwe imethibishwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS)” Sima alifafanua.
  • Amesisitiza busara itumike katika kumaliza mgogoro uliopo baina ya mfanyabiashara aliyeagiza bidhaa hiyo huo bila kuathiri upande wowote kwa kutoa mapendekezo kwa mfanyabiashara mwenye mzigo husika kuurejereza ama kuusafirisha nje ya chini ya uangalizi maalumu na kuagiza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Shirika la Viwango nchini (TBS) kumaliza suala hilo mapema iwezekanavyo.
33-01
Mmoja ya washiriki wa Mkutano akiwasilisha hoja yake mbele ya jopo la Mawaziri na Manaibu Waziri walioshiriki Mkutano  wa Mashauriano baina ya Serikali, Wafanyabiashra na Wawekezaji katika ukumbi wa Chuo cha Wauguzi Kibaha Pwani.
  • Katika hatua nyingine Naibu Waziri Sima amesema kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais imefanya mapitio ya Kanuni za Taka Hatarishi za mwaka 2009 na kutunga Kanuni mpya ya mwaka 2019 ambazo zimezingatia Mkataba wa Basel yaani Basel Convention for transboundary Movement of Hazadous Waste ambao Tanzania imeridhia baada ya awali biashara hiyo hairatibiwi ipasavyo
  • “Kwa mujibu wa Mkataba huu, mfanyabiashara anapotaka kuingiza Hazadous Waster ikiwemo chuma chakavu pamoja na masharti mengine ni lazima nchi ambapo chuma chakavu kinatoka kupata kibali cha Serikali ya nchi husika ili kuthibitisha kuwa nchi hiyo imeruhusu usafirishaji huo” Sima alisisitiza.
  • Amefafanua kuwa malighafi inayotumika na Viwanda vya ndani imekuwa ikipelekwa nje, hivyo Serikali imeweka masharti  magumu kwa lengo la kulinda viwanda vya ndani na kuruhusu kusafirishwa kwa malighafi ambayo haitumiki hapa nchini.
  • Naibu Waziri Sima amewahimiza wawekezaji kuwekeza katika Mkoa wa Pwani na kutumia nishati ya gesi kwa wingi. “Ni viwanda 48 tu nchi nzima ndio vinatumia nishati ya gesi, wawekezaji wekeni nia ya matumizi ya Gesi ili TPDC waweke miundombinu stahiki, nawasihi ndugu zangu tulinde mazingira yetu”
  • Siku ya pili ya mkutano wa Mkutano wa Mashauriano baina ya Serikali, Wafanyabiashara na Wawekezaji umefanyika katika ukumbi wa Chuo cha Uuguzi Kibaha mkoa wa Pwani na kuhudhuriwa na washiriki kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Pwani. Na Lulu Mussa ,Pwani

 

 

Ad

Unaweza kuangalia pia

TANZANIA YATAKA AMANI KUPUNGUZA MZIGO WA WAKIMBIZI AFRIKA

Tanzania imetaka Umoja wa Afrika na Jumuiya za Kimataifa kuongeza jitihada na nguvu katika kuleta …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *