BALOZI WA UJERUMANI NCHINI REGINE HESS ATEMBELEA TAASISI YA MOYO KWA AJILI YA KUONA KAMBI MAALUM YA MATIBABU YA MOYO KWA WATOTO

1111-01
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na Balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Regine Hess alipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuona kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanywa na wataalamu kutoka JKCI, Israel na Ujerumani. Kushoto ni Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka nchini Ujerumani Felix Berger.
2-01
Balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Regine Hess akizungumza na wataalamu wa afya wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Israel na Ujerumani alipotembelea JKCI kwa ajili ya kuona kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto wenye matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo. Katika kambi hiyo watoto 55 walifanyiwa uchunguzi wa moyo, kati ya hao 18 walifanyiwa upasuaji mdogo wa kuziba matundu na kuzibua mishipa ya damu ya moyo iliyoziba, saba watapelekwa nchini Israel kwa ajili ya matibabu yanayohitaji utaalamu wa hali ya juu zaidi na 30 watatibiwa hapa nchini.
1 -01
Balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Regine Hess akizungumza na mama wa mtoto aliyefanyiwa upasuaji mdogo wa moyo wa bila kufungua kifua kupitia tundu dogo linalotobolewa kwenye paja wa kuziba tundu la moyo katika kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanywa na madaktari bingwa wa Moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Israel na Ujerumani.

 

5 -01
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Regine Hess na wataalamu wa afya kutoja JKCI, Ujerumani na Israel mara baada ya balozi huyo kumaliza ziara yake ya kutembelea Taasisi hiyo ili kuona maendeleo ya kambi maalum ya matibabu ya moyo kwa watoto inayofanywa na wataalamu kutoka JKCI, Israel na Ujerumani. Katika kambi hiyo watoto 55 walifanyiwa uchunguzi wa moyo, kati ya hao 18 walifanyiwa upasuaji mdogo wa kuziba matundu na kuzibua mishipa ya damu ya moyo iliyoziba, saba watapelekwa nchini Israel kwa ajili ya matibabu yanayohitaji utaalamu wa hali ya juu zaidi na 30 watatibiwa hapa nchini.

 

Ad

Unaweza kuangalia pia

ONGEZENI KASI YA KUWAHUDUMIA WANANCHI – DKT. CHAULA

Watumishi wa afya nchini wametakiwa kuongeza kasi ya kuwahudumia wananchi kwenye vituo vya kutolea huduma …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *