Matokeo ChanyA+

Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+.

MAGARI YANAYOTUMIA GESI YAONGEZEKA NCHINI

  Serikali imebainisha kuwa matumizi ya gesi asilia katika magari nchini yamezidi kukua ambapo kwa sasa idadi imefikia 210 kutoka 65 yaliyokuwa yakitumia nishati hiyo, mwaka 2017. Hayo yalibainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dkt. James Mataragio, jijini Dodoma, leo Agosti 21, 2019  wakati …

Soma zaidi »

TANZANIA KUNUFAIKA NA DOLA BILIONI 1.7 KUTOKA BENKI YA DUNIA

Uhusiano wa Benki ya Dunia na Serikali ya Tanzania umeimarika baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo anayesimamia nchi 22 zilizoko Kanda ya Afrika, Bi. Anne Kabagambe, kumhakikishia Waziri wa Fedha na Mipango kuwa Benki hiyo iko tayari kutoa kwa Tanzania fedha zote za mkopo wa masharti nafuu kiasi cha …

Soma zaidi »

TANZANIA NI SALAMA KWA UWEKEZAJI – RC NDIKILO

Mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo ,amesisitiza kwamba, Tanzania hususan mkoani Pwani ni salama kwa uwekezaji na amekemea propaganda na uvumi unaoenezwa na baadhi ya watu wasiolitakia mema Taifa kuwa hakuna uwekezaji unaoendelezwa. Aidha amewaasa ,wawekezaji na wenye viwanda kuhakikisha wanasajili namba za utambulisho ya mlipa kodi (TIN …

Soma zaidi »

NCHI 60 KUSHIRIKI MAONYESHO YA UTALII TANZANIA

Zikiwa zimebaki siku 57 kufikia Tamasha kubwa la utalii hapa Nchini linalofahamika kama “Swahili International Tourism Expo” , Bodi ya utalii Tanzania TTB imethibitisha kuwa imejipanga vema kuwapokea wageni toka nchi 60 watakaoshiriki Tamasha hilo. Akizungumza na Waandishi wa Habari  Jijini Dar es Salaam leo , Mkurugenzi wa Bodi ya …

Soma zaidi »

MITAMBO YA KUNYANYULIA MIZIGO YA UJENZI WA MRADI WA JN HPP YAZINDULIWA RASMI FUGA

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe.Atashasta Nditiye amazindua Rasmi Vifaa vya Kunyanyulia Makontena ya Mizigo na Vifaa vizito vya utekelezaji wa ujenzi wa Mradi mkubwa wa umeme wa Julius Nyerere Hydro Power Project (JN HPP). Akizungumza jana katika stesheni ya fuga, Waziri Nditiye alisema kuwa Serikali imenunua vifaa …

Soma zaidi »

KISWAHILI LUGHA YA NNE RASMI KWA NCHI ZA SADC

Kiswahili kuwa lugha ya nne rasmi itakayotumika katika mikutano na machapisho mbali mbali ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Akitangaza katika Mkutano wa 39 wa Wakuu wa nchi na Serikali za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Mwenyekiti wa SADC Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania …

Soma zaidi »

RAIS MAGUFULI AKABIDHIWA UENYEKITI WA SADC

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 17 Agosti, 2019 amekabidhiwa Uenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC ulioanza leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere …

Soma zaidi »