Taarifa ya Habari

WAZIRI HASUNGA ATOA AGIZO KWA BODI ZA MAZAO KUKAMILISHA KANZI DATA ZA WAKULIMA IFIKAPO JUNI 30

Serikali imetoa agizo kwa Wakurugenzi wa Bodi za Mazao ya Kilimo nchini kukamilisha Kanzi Data ya wakulima wote itakayowawezesha wakulima hao kutambulika kwa urahisi. Agizo hilo limetolewa jijini Dodoma na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga wakati alipokuwa akipokea msaada wa vifaa mbalimbali vilivyotolewa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa …

Soma zaidi »

SERIKALI MBIONI KUANZA MPANGO WA UAGIZAJI WA GESI YA MITUNGI (LPG) KWA PAMOJA

Serikali imesema iko katika hatua za awali za kuandaa mpango  wa uagizaji wa gesi ya mitungi (LPG) kwa pamoja kama ilivyo kwa mafuta ya Petroli hali itakayosaidia kudhibiti masuala mbalimbali ikiwemo  bei ya gesi hiyo . Akizungumza wakati wa semina kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati …

Soma zaidi »

CREDIT SUISSE BANK: TUTAENDELEA KUIKOPESHA TANZANIA KWA KUWA INAKOPESHEKA NA MAHILI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI

Benki ya Credit Suisse ya Uingereza imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuikopesha Tanzania ili kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo baada kuridhishwa na uaminifu wa urejeshaji mikopo kwa wakati pamoja na ubora wa viwango vya miradi inayotekelezwa nchini. Ahadi hiyo imetolewa Mjini Washington D.C nchini Marekani na Mkurugenzi wa Masoko …

Soma zaidi »

NAIBU WAZIRI KWANDIKWA ASISITIZA MRADI WA NYUMBA ZA KISASA MAGOMENI KOTA UKAMILIKE DESEMBA 2019

NAIBU Waziri wa Ujenzi Mhe. Elias John Kwandikwa ameagiza Wakala wa Majengo Nchini (TBA) kuhakikisha wanamaliza Mradi wa Nyumba za Kisasa wa Magomeni Kota jijini Dar es Salaam unamalizika kufikia mwezi Desemba mwaka huu. Naibu Waziri wa Ujenzi Mhe. Kwandikwa ametoa msisitizo huo leo jijini Dar es Salaam alipofanya ziara …

Soma zaidi »

BENKI YA DUNIA KUTOA MKOPO NA MSAADA WA SHILINGI TRILIONI 4 KWA AJILI YA KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Benki ya Dunia imeahidi kuipatia Tanzania mkopo wenye masharti nafuu na msaada wenye thamani ya dola za Marekani bilioni 1.7 sawa na takriban shilingi trilioni 4 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020. Ahadi hiyo imetolewa mjini Washington …

Soma zaidi »

SERIKALI IMEJIPANGA KUHAKIKISHA MIFUKO MBADALA YA PLASTIKI INAPATIKANA KWA WINGI ILI KUKIDHI MAHITAJI

Serikali imefafanua tamko lake la kupiga marufuku uzalishaji, usambazaji na matumizi ya mifuko ya plastiki hapa nchini. Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba katika Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika Jijini Dodoma na kusisitiza kuwa katazo la Mifuko ya …

Soma zaidi »

WAZIRI KAIRUKI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA KENYA NCHINI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Kenya nchini Tanzania Mhe. Dan Kazungu mapema katika ofisi zake Jijini Dodoma. Lengo la mazungumzo hayo ilikuwa kujadili masuala mbalimbali ikiwemo namna ambavyo Kenya inavyoweza kushirikiana na Tanzania katika masuala ya uwekezaji ambapo …

Soma zaidi »