UCHAGUZI: Liwale kujitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya Jumamosi Oktoba 13 mwaka 2018.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewasihi wapiga kura wote waliojiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na wanaoishi kwenye Jimbo la Liwale mkoani Lindi na kata nne za Tanzania Bara, kujitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya Jumamosi Oktoba 13 mwaka huu ili kuwachagua viongozi wanaowataka wawaongoze kwa kipindi cha takribani miaka miwili ijayo.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Semistocles Kaijage wakati akisoma risala ya uchaguzi mdogo wa jimbo hilo unaohusisha pia kata za Kibutuka katika Halmashauri ya Liwale, kata ya Korongoni katika Halmashauri ya Manispaa ya Moshi na Kata za Majengo na King’ori katika Halmashauri ya Meru.

Amewataka kwenda kupiga kura bila hofu, woga, wasiwasi au ushawishi kwani chini ya Kanuni ya 3.1 (b) ya Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015, Serikali imepewa wajibu wa kuhakikisha kuwa kuna hali ya usalama, amani na utulivu katika kipindi chote cha Uchaguzi.

Mbali na wito huo, Jaji Kaijage amewataka wananchi, vyama vya Siasa na wadau wote wa uchaguzi kushirikiana ili kuhakikisha kuwa viashiria vya kuvunjika kwa amani na utulivu vinaepukwa ili uchaguzi utakaofanyika uwe huru, wazi na wa haki.

Jaji Kaijage amevisisitiza vyama vya siasa kuwa mikutano ya kampeni inatakiwa kufikia mwisho leo Ijumma saa kumi na mbili kamili (12:00) jioni na baada ya muda huo, vyama, wagombea na mashabiki waache kufanya kampeni za aina yoyote, kama vile kutumia alama za vyama zinazoashiria kampeni, vipeperushi, bendera, mavazina vitu vingine visivyokubalika katika siku ya Uchaguzi.

Ad

Unaweza kuangalia pia

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MKUTANO WA WOMENLIFT HEALTH

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akimsikiliza Maelezo kutoka kwa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *