Mkutano wa 18 wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa Nchi za Afrika na Nordic (Afrika 29 na 5 za Nordic)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli amefungua Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa Afrika-Nordic jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa JNICC.

Mada ya mkutano wa mwaka huu Ushirikiano kwa maendeleo endelevu.

Ad

Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiaano wa Kimataifa Profesa Palamagamba Kabudi amewaalika wenzake kadhaa wa Kiafrika na Nordic kwenye Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa Afrika-Nordic jijini Dar es salaam tarehe 8 Novemba, 2019.

Mkutano huo umehudhuriwa na mawaziri 29 wa kigeni wa nchi za Afrika na wengine watano kutoka nchi za Nordic ambazo ni Swiden, Denmark, Finland, Norway na Iceland.

Nchi za Afrika ambazo zimehudhuria mkutano huu ni Algeria, Angola, Benin, Botswana, Burkinafaso, Burundi, Comoros, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Misri, Ethiopia na Ghana.

Nchi zingine ni; Kenya, Lesotho, Mali, Malawi, Moroko, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Niger, Rwanda, Senegal, Somalia, Afrika Kusini, Tunisia, Uganda, Zambia, Zimbabwe na mwenyeji -Tanzania.

Mbali na mawaziri wa mambo ya nje mkutano huo pia umehudhuriwa na mabalozi wa nchi zinazoshiriki za Kiafrika na Kutoka katika nchi za Nordic.

Ushirikiano kwa Maendeleo Endelevu.

Screen Shot 2019-11-08 at 10.47.07.png

 

Ad

Unaweza kuangalia pia

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetenga zaidi ya shilingi bilioni 250 katika mwaka wa fedha 2024/25 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa na vifaa tiba kwa vituo vyote vya kutolea huduma za afya ya msingi katika Halmashauri zote 184 nchini

Taarifa hii imetolewa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI anayeshughulikia …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *