Jimbo la Guangdong limeahidi kutoa fursa kwa wafanyabiashara wa Tanzania kushiriki katika maonesho mbalimbali ya biashara yanayoandaliwa kwa ajili ya kutangaza bidhaa za Tanzania katika soko la China.
![BALOZI WA TANZANIA NCHINI CHINA ALETA FURSA KWA WAFANYABIASHARA NCHINI](https://matokeochanya.co.tz/wp-content/uploads/2018/10/CHN-3.png)
Ahadi hiyo imetolewa na kiongozi wa Serikali ya Jimbo hilo Ndugu Zheng Jianlong alipokutana na Balozi wa Tanzania nchini humo, Balozi Mbelwa Kairuki.
Ad
![BALOZI KAIRUKI NA KIONGOZI WA JIMBO LA GUANGDONG](https://matokeochanya.co.tz/wp-content/uploads/2018/10/CHN-1-2350997321-1539336100934.png)
Hii ni fursa kwa wafanyabiashara nchini kwenda kutangaza bidhaa za ndani za kilimo, madini na utalii ili kuweza kupata wawekezaji na soko bora na la uhakika kutoka nchi hiyo.
Ad