MAAFISA TARAFA MKOANI RUKWA WAKABIDHIWA PIKIPIKI ILI KUBORESHA UTENDAJI KAZI

Katika hatua za kuboresha utendaji kazi wa Maafisa Tarafa nchini Rais Wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John pombe Magufuli ametoa pikipiki 12 kwa Maafisa Tarafa mkoani Rukwa ili ziweze kuwasaidia kutekeleza majukumu yao ya kiserikali katika kata wanazozihudumia.

Pikipiki hizo zimetolewa ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa tarehe 04.06.2019 baada ya kufanya kikao kazi na Maafisa Tarafa wote nchini alipokutana nao Ikulu Jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi pikipiki hizo Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alimshukuru Rais kwa kutimiza ahadi hiyo huku akiwasisitiza maafisa hao kuzitumia pikipiki hizo kwa malengo yaliyokusudiwa na Rais ikiwemo kusimamia mapato, miradi ya maendeleo iliyopo kwenye maeneo yao pamoja na kusikiliza kero za wananchi.

Uongozi wa Mkoa wa Rukwa ukiongozwa na Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Tarafa wa mkoa baada ya makabidhiano ya Pikipiki zilizotolewa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli.


Alieleza kuwa katika ziara zake alizozifanya katika maeneo ya vijijini, alibaini kuwepo kwa mwamko mdogo wa wananchi juu ya ugonjwa hatari wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19) hivyo kuwataka maafisa hao kuhakikisha wanavitumia vyombo hivyo kufikisha elimu ya ugonjwa huo hatari.

“Ni Imani yangu kuwa tutavitumia vyombo hivi vya usafiri kuhakikisha kuwa tunawafikia wananchi wetu kwenye maeneo yao ili tuweze kuwahamasisha kujikinga na ugonjwa huu hatari ikiwa ni pamoja na kuvaa barakoa, kunawa mikono kwa maji tiririka mara kwa mara na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima,” Alisema

Aidha, Alimtaka Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa kuhakikisha anachukua hatua kali za kisheria na kiutumishi kwa Afisa Tarafa yeyote atakayetumia pikipiki hiyo kinyume na malengo ya serikali ikiwemo kutumia kama Bodaboda na kuongeza kuwa pikipiki hizo zina namba za serikali, hivyo, kuzitumia kinyume na malengo yake ni ukosefu wa maadili.

Ad
Ad

Unaweza kuangalia pia

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MKUTANO WA WOMENLIFT HEALTH

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akimsikiliza Maelezo kutoka kwa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *