MRADI HUU NI MATOKEO CHANYA YA MIRADI INAYOFANYA NA SERIKALI – RAIS MAGUFULI

Muonekano wa jengo la kituo kipya cha mabasi wa mkoani linaloendelea kujengwa katika eneo la Mbezi Luis jijini Dar Es Salaam
Rais Dkt. John Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwa katika picha na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Juu katika Makutano ya Ubungo (Ubungo flyovers)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Mhe. Rais wa Malawi, Dkt. Lazarus Chakwera wakifungua pazia la jiwe la msingi la ujenzi wa kituo cha kisasa cha mabasi kilichopo Mbezi Luis, Dar es salaam leo Oktoba 8, 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na akizunguma na Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Palamagamba Kabudi, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi na wa miwsho kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Aboubakar Kunenga wakati wa uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa kituo cha kisasa cha mabasi kilichopo Mbezi Luis, Dar es salaam leo Oktoba 8, 2020.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Malawi Mheshimiwa Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera wameweka jiwe la msingi la ujenzi wa stendi Kuu ya Mabasi yaendayo Mikoani na nchi jirani , eneo la Mbezi mwisho Jijini Dar es Salaam leo tarehe 08 Oktoba 2020.

Akizungumza katika hafla hiyo Rais Magufuli amesema kuwa stendi hiyo iwekwe ofisi ya Uhamiaji kwani stendi hiyo ni ya kimataifa na kuongeza kuwa katika kupangwa kwa eneo hilo kuwekwe eneo la mabasi yanayotoka nje ya nchi ili kurahisisha kutoa huduma.

Ad

“Mabasi yanatoka nje ya nchi yawe na sehemu yao ya maengesho, mabasi ya humu yawe na sehemu yao, daladala yawe na sehemu yao, bajaji ziwe na sehemu yao, mama lishe wawe na sehemu zao, hapo pataweza kuleta umaana wa stendi hii na hapo unaweza ukaleta umaana wa fedha za walipa kodi ambao ambao ni watanzania wote” amesema Rais Magufuli

Aidha, Rais Magufuli amesema kuwa amefurshishwa kushuhudia mradi huo kwani mradi huo ni “MATOKEO CHANYA ya miradi inayofanywa na Serikali.

Ad

Unaweza kuangalia pia

BANDARI YA DAR ES SALAAM INAPANUKA NA KUIMARIKA: HATUA MUHIMU KWA UCHUMI WA TANZANIA

Bandari ya Dar es Salaam ni kitovu muhimu cha biashara na uchumi wa Tanzania, na …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *