KIKAO CHA MAKATIBU WAKUU WA SADC KIKIENDELEA

Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wameendelea na kikao chao kwa siku ya pili ikiwa ni maandalizi ya mkutano wa baraza la mawaziri wa SADC unaotarajiwa kufanyika tarehe 12 – 13 Machi, 2021 kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam.   

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiwasilisha mada katika kikao cha Makatibu Wakuu wa SADC kinachoendelea jijini Dar es Salaam kwa njia ya mtandao. Kikao hicho ni maandalizi ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC utakafanyika tarehe 12, Machi kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam.

Ujumbe wa Tanzania katika kikao hicho unaongozwa na Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Shaban.   

Ad
Washiriki wa kikao cha makatibu wakuu wakifuatilia kikao kinachoendelea kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam

Mkutano wa Baraza la Mawaziri ujumbe wa Tanzania utaongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Africa Masahariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) ataongoza ujumbe wa Tanzania.

Kikao kikiendelea

Mwenyekiti wa Sasa katika Jumuiya ya SADC ni msumbiji na ndiye atakayeongoza majadiliano ya Mkutano huu.

Ad

Unaweza kuangalia pia

HERI YA SIKU YA WAFANYAKAZI, MEI MOSI

Tunawatakia Watanzania wote Heri ya Siku ya Wafanyakazi, Mei Mosi! Ni siku muhimu ya kuenzi …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *