MAWAZIRI SADC – TROIKA WAKUTANA KWA DHARURA BOTSWANA

Baraza la Mawaziri wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama wakutana katika mkutano wa dharura na kujadili masuala ya siasa, ulinzi na usalama.

Ujumbe wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) ukiwa ukiimba wimbo wa SADC kabla ya kuanza kwa mkutano wa dharura wa baraza la Mawaziri

Mkutano huo umefanyika leo mjini Gaborone, Botswana ambapo ulitanguliwa na mkutano wa Makatibu Wakuu wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ulioanza asubuhi na kumalizika mchana.

Ad

Kupitia mkutano huo, mawaziri wameweza kujadili masuala ya hali ya siasa, ulinzi na usalama katika kanda ya SADC na kupendekeza njia mbalimbali za kukabiliana na changamoto zinazojitokeza kwenye siasa, ulinzi na usalama ndani ya ukanda wa SADC.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Botswana Dkt. Lemogang Kwape akifungua mkutano wa Dharura wa baraza la mawaziri, kushoto kwake ni Katibu Mtendaji wa SADC, Dkt. Stegomena Taxi

Pamoja na mambo mengine, Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama  inawajibika kukuza amani na usalama katika eneo la SADC na pia ina wajibu wa kuongoza na kuzipatia nchi Wanachama mwongozo kuhusu mambo ambayo yanatishia amani, ulinzi na usalama.

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mtendaji wa SADC, Dkt. Stegomena Taxi mara baada ya kumaliza mkutano wao
Ad

Unaweza kuangalia pia

Serikali ya Tanzania na Czech Zakubaliana Kuondoa Utozaji Kodi Mara Mbili

Serikali za Tanzania na Czech kukuza ushirikiano wa kiuchumi na kuvutia uwekezaji kati yao. Kuondoa …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *