Jengo Jipya la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja likiwa katika Ujenzi wake katika eneo la hospitali hiyo.

RAIS Dk. SHEIN ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA JENGO LA HOSPITAL YA KIVUNGE

Rais wa Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisisitiza jambo wakati akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Afya Zanzibar, wakati alipotembelea Mradi wa Jengo la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja. kulia Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohammed na kushoto Daktari Dhamana wa Hospitali ya Kivunge Dr. Tamim Hamad Said na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Bi. Asha Abdallah.
Rais Dkt. Shein
Daktari Dhamani wa Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja Dr. Tamim Hamad Said, akitowa maelezo ya michoro ya jengo jipya la Hospitali ya Kivunge kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, wakati alipotembelea Mradi huo wa Ujenzi wa Hospitali hiyo katika eneo la Hospitali ya Kivunge.
Rias wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akielekezwa na kuonesha moja ya sehemu ya jengo hilo na Kaimu Mkurugenzi Tiba Wizara ya Afya Zanzibar na Dr. Fadhil Abdallah wakati akitembelea Mradi huo wa Ujenzi wa Hospitali Mpya ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Jengo jipya la hospital ya Mkoa
Jengo Jipya la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja likiwa katika Ujenzi wake katika eneo la hospitali hiyo.
Ad

Unaweza kuangalia pia

Matumizi ya Nishati Mbadala kwa Kupikia na Shughuli Nyingine Zafungua Mustakabali Mpya wa Kimazingira Tanzania

Kutumia nishati mbadala kwa kupikia na shughuli nyingine ni muhimu sana kwa Tanzania kutokana na …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *