Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, kuanza ziara ya kikazi mkoani Kigoma kwa siku nne.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 8 Septemba, 2018 anatarajiwa kuanza ziara ya kikazi ya kukagua na kuhimiza shughuli za maendeleo mkoani Kigoma kwa siku nne.

Mara atakapowasili mkoani Kigoma atapokea Taarifa ya Maendeleo ya Mkoa. Aidha, tarehe 9 Septemba, Makamu wa Rais atashiriki katika Sherehe za kuwekwa Wakfu Askofu Mkuu Msaidizi na Maaskofu wengine wanne wa majimbo katika kanisa la Pentekoste Motomoto Mwanga.

Ad

Tarehe 10, Makamu wa Rais atatembelea mwalo wa Muyobozi, atakagua ujenzi wa kituo cha Afya Uvinza na kuhutubia wananchi katika kijiji cha Kazuramimba.

Makamu wa Rais atahitimisha ziara yake tarehe 11, kwa kutembelea Wilaya ya Buhigwe ambapo pamoja na mambo mengine atazungumza na Wananchi wa Buhigwe katika eneo la Munzeze.

Ad

Unaweza kuangalia pia

NINAWASIHI MUWE NA SUBIRA WAKATI SERIKALI IKIIMARISHA MIFUMO YAKE YA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU – WAZIRI ZUNGU

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Azzan Zungu …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *