Barabara za juu katika eneo la Tazara jijini Dar es Salaam nchini Tanzania zimeanza kutumika hii leo kwa majaribio ambapo uzinduzi rasmi utafanyika baada ya tarehe rasmi kupangwa.
Akizungumza mara baada ya kufanyika kwa uzinduzi huo wa majaribio injinia Patrick Mfugale ambaye barabara hizo zimepewa jina lake Mfugale Fylover amesema kuwa hatua hiyo imepunguza foleni kwa kiasi kikubwa
Hata hivyo kituo cha abiria kilichohamishwa kimeleta usumbufu kwa wananchi
Akifafanua kuhusu vituo vya kushusha abiria injinia Mfugale amesema vituo rasmi katika eneo la Tazara vitapangwa vizuri baadaye.
Wananchi nao wamepongeza juhudi za Mheshimiwa Rais Dkt John Pombe Magufuli