Mandhari ya nje ya Maktaba hiyo kama inavyoonekana.

MAKTABA YA KISASA YAFUNGULIWA UDSM

Rais wa Jamhuri ya Muungano
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Balozi wa China hapa nchini Wang Ke wakati wakiagana mara baada ya hafla ya ufunguzi wa Maktaba hiyo ya Kisasa.
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amefungua maktaba mpya, kubwa na ya kisasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam iliyojengwa katika Kampasi Mlimani (Mwl. Julius K. Nyerere) Jijini Dar es Salaam.
  • Maktaba hiyo kubwa Afrika Mashariki na Kati imejengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 93.6 ikiwa ni msaada kutoka Serikali ya China na inakuwa maktaba kubwa kuliko maktaba zote ambazo China imezijenga barani Afrika.
RAIS MGUFULI AKICHEZA DANCE
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Balozi wa China hapa nchini Wang Ke wakicheza pamoja na kwaya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mara baada ya hafla ya ufunguzi wa Maktaba hiyo ya Kisasa.
  • Katika taarifa yake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. William Anangisye amesema majengo ya maktaba hiyo yenye ghorofa mbili yamechukua eneo lenye ukubwa wa meta za mraba 20,000 yakiwa na uwezo wa kuhifadhi vitabu 800,000, kukalisha watumiaji 2,100 kwa wakati mmoja, yana kompyuta 160 zilizounganishwa na mtandao kwa ajili ya kusoma vitabu kwa njia ya kielektroniki, ofisi za wafanyakazi, eneo la wanafunzi wenye mahitaji maalum na ukumbi wa kisasa wa mihadhara wenye uwezo wa kuchukua watu 600.
  • Prof. Anangisye ameishukuru Serikali kwa mchango mkubwa uliosaidia kufanikisha ujenzi wa maktaba hiyo, ameishukuru Serikali ya China kwa kutoa msaada wa fedha za ujenzi huo na kampuni ya ujenzi ya Jiangsu Jiangdu ya China kwa kujenga majengo yenye ubora na hadhi ya hali ya juu.
RAIS AKISALIMIANA NA LOWASSA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Msataafu Edward Lowassa mara baada ya kuwasili katika eneo la Maktaba mpya katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
  • Ameahidi kuwa Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam itahakikisha majengo ya maktaba hiyo yanatunzwa vizuri na maktaba inatumika kuwanufaisha wanafunzi wa chuo hicho pamoja na wanafunzi wa taasisi zingine za vyuo na wananchi wa kawaida.
 Mandhari ya nje ya Maktaba hiyo kama inavyoonekana.
Mandhari ya nje ya Maktaba hiyo kama inavyoonekana.
SISI-NI-TANZANIA-MPYA---306
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisoma moja ya kitabu cha Sayansi katika maktaba hiyo mpya.
  • Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa namna anavyotoa kipaumbele kwa sekta ya elimu na ameahidi kuwa wizara yake itaendelea kuhakikisha taasisi zote zilizo chini ya wizara hiyo zinaendeshwa kwa kuzingatia maadili na matumizi bora ya rasilimali, pia amemshukuru Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke kwa kusimamia na kufuatilia kwa ukaribu ujenzi wa maktaba hiyo na kwa Serikali ya China kutoa shilingi Bilioni 50.8 kwa ajili ya ujenzi wa chuo cha elimu ya mafunzo ya ufundi stadi (VETA) Mkoani Kagera.
RAIS AKIPOKE ZAWADI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea zawadi ya Vitabu kutoka kwa Balozi wa China hapa nchini Wang Ke kabla ya ufunguzi wa Maktaba hiyo.
  • Akizungumza katika sherehe hizo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemshukuru Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke na kumuomba apeleke shukrani za Tanzania kwa Rais wa China Mhe. Xi Jinping kwa misaada ambayo China imekuwa ikiitoa kwa Tanzania, ikiwemo ujenzi wa Maktaba hiyo na Chuo cha VETA kitakachojengwa Mkoani Kagera.
  • Mhe. Rais Magufuli amesema urafiki wa China na Tanzania ulioasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Mwenyekiti Mao Zedong umeendelea kuleta manufaa makubwa na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano na itauendeleza na kuukuza uhusiano na ushirikiano huu mzuri.
Dkt. John Pombe Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia katika hafla hiyo ya ufunguzi wa Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
  • “Jambo la kufurahisha ni kwamba misaada yao haiambatani na masharti. Wenyewe wakiamua kukupa wanakupa, walitujengea TAZARA, URAFIKI na pia wametusaidia katika maeneo mengine ya maendeleo” amesema Mhe. Rais Magufuli na kumhakikishia Mhe. Balozi Wang Ke kuwa Serikali itahakikisha kila msaada unaotolewa unatumiwa vizuri.
  • Aidha, Mhe. Rais Magufuli amempongeza Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Mstaafu Prof. Rwekaza Mukandala kwa kuandaa mpango wa ujenzi wa maktaba hiyo, na pia amewapongeza Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kupata maktaba ambayo itawasaidia kuongeza kiwango cha ubora wa elimu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelezo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelezo mbalimbali ya maktaba hiyo mpya itakavyokuwa ikihudimia wanafunzi na wadau mbalimbali wa elimu watakapoanza kuitumia.
  • Amewataka wana Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuhakikisha maktaba hiyo inatunzwa vizuri na ametoa wito kwa Watanzania kujifunza lugha ya Kichina katika jengo mojawapo la maktaba hiyo litakalokuwa likifundisha lugha hiyo kwa kuwa kuna manufaa makubwa kwa Watanzania kujifunza lugha hiyo.
RAIS AKIPATA MAELEKEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelezo mbalimbali ya maktaba hiyo mpya itakavyokuwa ikihudimia wanafunzi na wadau mbalimbali wa elimu watakapoanza kuitumia.
  • Sherehe hizo zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, Mawaziri Wakuu Wastaafu Mhe. Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba na Mhe. Edward Ngoyai Lowassa, Mawaziri, Mabalozi wa nchi mbalimbali na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda.
NDANI YA MAKTABA
Taaswira ya moja ya Mashelfu yenye vitabu katika maktaba hiyo mpya.
TASWIRA
Taaswira ya moja ya Mashelfu yenye vitabu katika maktaba hiyo mpya.
MAELEKEZO YAKITOLEWA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia moja ya kompyuta zinazohifadhi vitabu (onlinebooks) ambazo wanafunzi watakuwa wakijisomea pamoja na kupata huduma ya mtandao internet.
RAIS NA BALOZI WA CHINA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akirudisha kitabu hicho kwenye shelfu la vitabu mara baada ya kukisoma huku Balozi wa China hapa nchini Wang Ke akiangalia.
SISI-NI-TANZANIA-MPYA---295
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kisoma huku Balozi wa China hapa nchini Wang Ke akiangalia.
Rais akionyesha funguo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea mfano wa funguo kutoka kwa Balozi wa China hapa nchini Wang Ke kuashiria ufunguzi wa Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 2100 kwa wakati mmoja huku viongozi wengine wakipiga makofi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe pamoja na Balozi wa China hapa nchini Wang Ke kuashiria ufunguzi wa Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 2100 kwa wakati mmoja. Wengine katika picha wanaoshuhudia ni Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba, Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Mama Kate Kamba, Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo cha Dar es Salaam Profesa William Anangisye
Ad

Unaweza kuangalia pia

LIVE: UZINDUZI WA MAJENGO YA OFISI YA MANISPAA NA MKUU WA WILAYA KIGAMBONI JIJINI DSM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 11, Febuari, …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *