Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasha Trekta aina ya Ursus wakati alipozindua matrekta mawili yatakayosaidia kuinua kilimo cha michikichi katika Gereza la Kwitanga mkoani Kigoma
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua matrekta mawili aina ya Ursus yenye thamani ya shilingi milioni 145 yatakayosaidia kuinua kilimo cha michikichi katika Gereza la Kwitanga mkoani Kigoma Februari 17, 2019. Wengine kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamadi Masauni, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi Stella Manyanya, Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali Mstaafu, Emmanuel Maganga.
Kiwanda cha Kuunganisha Trekta za Ursus ni kiwanda kinachosimamiwa na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) ambapo huunganisha Trekta zinazokuja kwa vipande kutoka nchini Poland. Kiwanda hicho kilianza rasmi kufanya kazi Aprili, 2017 ambapo ni moja ya matunda ya kauli mbiu ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya ujenzi wa viwanda.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mashine ya kukamua mafuta ya mawese wakati alipotembelea Gereza la Kwitanga mkoani Kigoma ambalo ni maarufu kwa kilimo cha michikichi.Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipanda mchikichi ikiwa ni ishara ya kuzindua mpango wa kupanua mashamba ya michikichi katika Gereza la Kwitanga mkoani Kigoma