RAIS MAGUFULI PAMOJA NA MARAIS WASTAAFU WAWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA OFISI ZA IKULU YA CHAMWINO, DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere wakivuta utepe kuashiria uwekaji wa Jiwe la Msingi Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mhe. Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo tarehe 30 Mei, 2020 wameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ofisi Kuu za Ikulu, Mkoani Dodoma.

Majengo 6 ya Ofisi za Ikulu yaliyounganishwa yanajengwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) katika eneo la Vikonje Jijini Dodoma kwa usanifu na muonekano sawa na majengo ya Ofisi za Ikulu Jijini Dar es Salaam, na yanatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi 5 ijayo.

Ad
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere wakivuta utepe kuashiria uwekaji wa Jiwe la Msingi Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020.

Ujenzi wa majengo ya ofisi hizo ni sehemu ya ujenzi mkubwa wa Ikulu Mkoani Dodoma, na tayari majengo mengine mbalimbali ikiwemo nyumba ya makazi ya Rais, Ofisi mbalimbali na uwigo wa ukuta (Fence) wenye urefu wa kilometa 27 yamekamilika na yanatumika.

Katika hotuba yake, Mhe. Rais Magufuli amelipongeza Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa kazi nzuri ya ujenzi wa Ofisi hizo pamoja na majukumu mengine ya ujenzi na uzalishaji mali wanayoyatekeleza, na ameeleza kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono jitihada hizo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere wakivuta utepe kuashiria uwekaji wa Jiwe la Msingi Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020.

Rais Magufuli ameipongeza Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA) ambayo ni mkandarasi mshauri wa mradi huo na amemuagiza Waziri wa Fedha Dkt. Philip Mpango kutoa shilingi Bilioni 2 zitakazoungana na shilingi Bilioni 1 zilizotolewa awali ili JKT kupitia shirika lake la SUMA-JKT wakamilishe ujenzi katika kipindi cha miezi 5 walioahidi.

Mhe. Rais Magufuli amewashukuru Mama Maria Nyerere na Marais Wastaafu kwa kuhudhuria sherehe za uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi hizo na kutembelea maeneo ya Ikulu ya Chamwino ambapo wamejionea kazi iliyofanyika kujenga miundombinu na majengo ikiwemo makazi ya Rais.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshika Chepe ili kuweka zege na Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa kuashiria uwekaji wa jiwe la Msingi Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshika Chepe ili kuweka zege na Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa kuashiria uwekaji wa jiwe la Msingi Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020.

Rais Magufuli ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano iliamua kuchukua hatua madhubuti za kutekeleza azimio la Serikali kuhamia Dodoma kama alivyoahidi mwezi Julai 2016 ambapo tayari Wizara zote, watumishi, viongozi wakuu akiwemo yeye mwenyewe wamehamia Dodoma, na kwamba kutokana na mafanikio hayo ameona ni vema jengo kuu la Ofisi za Ikulu lijengwe kwa mfano uleule wa Ikulu ya Dar es Salaam ili kutunza historia.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Marais Wastaafu, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere mara baada ya chakula cha mchana katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.

Aidha, Rais Magufuli amesema Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere alipotangaza uamuzi wa kuhamia Dodoma na kujenga Ikulu ya Chamwino, alichukua eneo la ekari 61 ambalo lilikuwa ni kubwa zaidi ya ekari 41 za Ikulu ya Dar es Salaam, lakini baada ya yeye kuamua kutekeleza uamuzi huo ameongeza eneo hadi kufikia ekari 8,473, amejenga kilometa 27 za ukuta wa kuzunguka eneo lote, amejenga barabara za lami na ameweka wanyama mbalimbali wakiwemo pundamilia, twiga, swala, sungura pori, kudu, batamaji na aina mbalimbali za ndege.

Mhe. Rais Magufuli amebainisha kuwa ukubwa wa Ikulu ya Chamwino (ekari 8,473) ni zaidi ya mara 15 ya ukubwa Hifadhi ya Taifa ya Saanane yenye ukubwa ekari 533 na kwamba kutokana na uwepo wa wanyamapori na mandhari ya kuvutia, Ikulu ya Chamwino inaweza kutumika kama kivutio cha utalii

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Marais Wastaafu, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere pamoja na viongozi wengine wakati wa wimbo wa Taifa.

Katika salamu zao, Waheshimiwa Marais wastaafu na familia ya Baba wa Taifa (salamu zimewasilishwa na Ndg. Makongoro Nyerere) wamempongeza na kumshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kuhamisha Serikali yote kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma pamoja na kujenga majengo na miundombinu mbalimbali ya Ikulu, Chamwino ikiwemo Ofisi Kuu ya Ikulu.

Sherehe hizo, zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Spika wa Bunge Mhe. Job Yustino Ndugai, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Ibrahim Hamis Juma, Mawaziri Wakuu Wastaafu (Mhe. John Samwel Malecela na Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda), Mawaziri, Katibu Mkuu Kiongozi, Makatibu Wakuu, Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (Bara) Ndg. Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Bashiru Ally Kakurwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo la Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete mara baada ya kuweka jiwe la msingi Ujenzi wa Ikulu ya Chamwino.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere wakielekea kwenye uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Ofisi za Ikulu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli pamoja Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere wakisikiliza maelezo kuhusu ujenzi wa Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli pamoja Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere wakisikiliza maelezo kuhusu ujenzi wa Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na vijana wa JKT wanaojenga Ikulu ya Chamwino.

Mapema, Mama Maria Nyerere (kwa niaba ya Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere), Rais Mstaafu Mwinyi, Rais Mstaafu Mkapa na Rais Mstaafu Kikwete walikabidhiwa ndege aina ya Tausi 25 na kilo 100 za chakula cha Tausi kwa kila mmoja kwa ajili ya kwenda kuwafuga katika bustani zao. Viongozi hao waandamizi wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuwapa ndege hao.

Ndege aina ya Tausi ambao waliletwa nchini na Baba wa Taifa hayati Mwl. Nyerere wameongezeka kwa idadi kubwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kutoka 403 hadi 2,260 na hivi sasa wanawekwa katika Ikulu ndogo za hapa nchini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia bendi ya ya JKT mara baada ya hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020. PICHA NA IKULU
Ad

Unaweza kuangalia pia

PROF. KABUDI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA MABALOZI WA UFARANSA, UTURUKI NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Pamalagamba Kabudi amekutana na …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *