RAIS MAGUFULI AKABIDHI NDEGE AINA YA TAUSI KWA MARAIS WASTAAFU KATIKA IKULU YA CHAMWINO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Hati ya Makabidhiano ya zawadi ya Ndege aina ya Tausi 25 kwa Mama Maria Nyerere mjane wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kwa ajili ya kuwafuga katika Makazi yake, hafla hiyo fupi ilifanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi hao Wakuu wastaafu mara baada ya kuwakabidhi zawadi ya ndege aina ya Tausi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete mara baada ya hafla fupi ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi katika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza katika hafla hiyo fupi ya Makabidhiano ya zawadi ya ndege aina ya Tausi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete wakati akitoa neno la Shukrani kwa niaba ya Marais wenzake wastaafu. PICHA NA IKULU
Ad

Unaweza kuangalia pia

PROF. KABUDI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA MABALOZI WA UFARANSA, UTURUKI NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Pamalagamba Kabudi amekutana na …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *