Serikali ya Ufaransa imeahidi kutoa Euro milioni 150 sawa na shilingi bilioni 413 kwa ajili ya kuendeleza mradi wa awamu ya tano wa ujenzi wa mradi wa mabasi ya mwendokasi jijini Dar es Salaam.
Ahadi hiyo imetolewa na Balozi wa Ufaransa hapa nchini, Mhe. Frederic Clavier wakati alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi, (Mb) katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.
Prof. Kabudi amesema kuwa mazungumzo yake na Mhe. Clavie yalijikita katika utekelezaji wa mambo waliyokubaliana wakati alipofanya ziara ya kikazi mwezi Februari nchini Ufaransa.